Bondia Fancis Cheka kulia akiwa amekingiana ngumi na bondia kutoka nchini Iran, Gavad Zahrevand wakati wa kupima uzito katika Ukumbi wa Idara ya habari Maelezo Dar es Salaam.

Bondia Sukkasem Kietyongyuth kushoto akiwa na kocha wake Win Panyaparichot wakati wa upimaji uzito
Bondia Fransic Miyeyusho 'Chichi Mawe' akipima uzito kwa ajili ya mpambano wake utakaofanyika PTA Sabasaba April 12 siku ya jumamosi.
Bondia Sukkasem Kietyongyuth kutoka Thailand akitunishiana misuli na Fransic Miyeyusho baada ya kupima uzito leo kwa ajili ya mpambano wao wa jumamosi ya April 12 katika ukumbi wa PTA Sabasaba Dar es Salaam.
 Bondia Fransic Cheka akipima uzito kwa ajili ya mpambano wake wa kesho April 12 katika ukumbi wa PTA Sabasaba kushoto ni bondia Gavad Zohrehvand wa Iran.  

Waandishi wa Habari wakipata taswira.
---
Na Mwandishi Wetu

 Bondia Fransic Miyeyusho 'Chichi' Mawe na  Bondia Sukkasem Kietyongyuth kutoka Thailand wamepima uzito kwa ajili ya mpambano wao utakaofanyika jumamosi ya April 12 katika ukumbi wa PTA Sabasaba.

Mpambano huo wa raundi kumi utasindikizwa na mabondia Fransic Cheka na bondia Gavad  Zohrehvand wa Iran atakaecheza raundi 8 mbali na mapambano hayo kutakuwa na mpambano mwingine utakaowakutanisha mabondia Ibrahimu Class 'King Class Mawe' atakae pambana na Mustafa Doto mpambano wa Raundi sita pia kutakuwa na mapambano mengi ya utangulizi yatakayosindikiza mchezo huo katika ukumbi wa PAT Sabasaba Dar es Salaam.
Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: