Meneja Uhusiano wa Nje wa Vodacom Tanzania Salum Mwalim akiongea na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa huduma ya kulipia mafuta kwa Mpesa kwenye vituo vya mafuta vya Total nchini. Kulia ni Mkurugenzi wa Biashara wa Total Romee de Villeneuve. Uzinduzi huo umefanyika leo jijini Dra es salaam.
 Meneja Uhusiano wa Nje wa Vodacom Tanzania,Salum Mwalim akiwaonesha waandishi wa habari (hawapo pichani) jinsi ya kulipia mafuta kwa Mpesa kwenye vituo vya mafuta vya Total muda mfupi baada ya kuzinduliwa rasmi kwa huduma hiyo kwenye kituo cha Total cha Morocco jijini Dra es salaam. Kulia ni Mkurugenzi wa Biashara wa Total Romee de Villeneuve. Huduma hiyo itakuwa ikipatikana kwenye vituo vyote vya Total hapa nchini.
 Meneja Uhusiano wa Nje wa Vodacom Tanzania Salum Mwalim (wa pili kushoto) akimsadia dereva Taxi Said Juma kulipia mafuta kwa njia ya M-pesa katika kituo cha Mafuta cha Totola Morocco jijini Dar es salaam akiwa ndie mteja wa kwanza kutumia huduma hiyo muda mfupi baada ya kuzinduliwa kituoni hapo. Kushoto ni Mkurugenzi wa Biashara wa Total Romee de Villeneuve na kulia ni mhudumu wa kituo hicho Malaki Peter. Huduma hiyo itakuwa ikipatikana kwenye vituo vyote vya Total nchini.
 Wafanyakazi wa Vodacom wa idara ya mauzo wakibandika stika kwenye kituo cha mafuta cha Total Morocco jijini Dar es salaam zinazoonesha nambari ya biashara ya kulipia huduma ya mafuta kwa njia ya Mpesa kituoni hapo. Huduma hiyo imezinduliwa kituoni hapo na kwamba itapatikana kwenye vituo vyote vya Total nchi nzima ikiwa ni mwendelezo wa Vodacom kuwawezesaha watanzania kupata huduma kwa urahisi, uhakika na usalama kupitia huduma ya M-pesa.
Mfanyakazi wa kituo cha mafuta cha Total Morocco jijini Dar es salaam akitoa huduma ya mafuta kwa wateja. Total na Vodacom imezindua ubia wa kibiashara unaowawezesha wateja kulipia huduma ya mafuta kwa M-pesa kwenye vituo vyote vya Total nchi nzima. Huduma hiyo inalenga kutoa unafuu na urahisi wa malipo kwa wateja.
Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: