Mkurugenzi wa Facebook wa Ushirikiano na Ukuaji wa Kimataifa, Bw. Nicola D’Elia akiongea katika uzinduzi huo uliofanyika jijini Dar es Salaam. Pembeni ni Mkurugenzi Mkuu wa Tigo, Bw. Diego Gutierrez (kushoto).
Mkurugenzi Mkuu wa Tigo, Bw. Diego Gutierrez (kushoto) akiwa amekumbatia na Mkurugenzi wa Facebook wa Ushirikiano na Ukuaji wa Kimataifa, Bw. Nicola D’Elia mara baada ya kumaliza uzinduzi uliofanyika jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mkuu wa Tigo, Bw. Diego Gutierrez (kushoto) na Mkurugenzi wa Facebook wa Ushirikiano na Ukuaji wa Kimataifa, Bw. Nicola D’Elia wakionyesha alama ya 'POA' mara baada ya kumaliza uzinduzi uliofanyika jijini Dar es Salaam.
Watu waliofika katika uzinduzi huo.
---
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam.

Kampuni ya simu ya mkononi TIGO  imetangaza kuingia katika ushirikiano na kampuni ya mtandao wa kijamii Facebook ambapo wateja wake wote nchini watapata huduma ya Facebook bure kwa lugha ya Kiingereza na kwa mara ya kwanza, katika lugha ya Kiswahili kupitia simu zao za mkononi.

Hii ni mara ya kwanza kwa Facebook kupatikana bila malipo kwa mtandao wowote eneo la Afrika mashariki, kwa mujibu wa Mkurugenzi Mkuu wa Tigo, Diego Gutierrez.

Akizungumza katika tafrija ya uzinduzi wa ushirikiano huo jijini Dar es Salaam, Gutierrez alisema: “Ushirikiano huu unamaanisha kwamba wateja wa Tigo kwa mara ya kwanza watakuwa na uwezo wakutumia Facebook kupitia simu zao za mkononi bila kukatwa gharama yeyote katika utumiaji wa data, hivyo kuwawezesha kuungana na watumiaji wapatao milioni 2 wa mtandao huo wa kijamii waliopo nchini Tanzania kati ya watumiaji bilioni 1.2 duniani kote.”

Gutierrez aliongeza: “Hii ni kwa mara ya kwanza mtandao wowote mkubwa wa kijamii umeweza kupatikanika kwa Kiswahili, lugha ya taifa inayotumika na Watanzania na wingi wa watu walio katika kanda ya Mashariki, Kati na Kusini mwa Afrika. ”

“Facebook imekuwa chachu kubwa ya utumiaji wa data kwa mitando ya simu. Kwa ushirikiano huu wa kipekee, Tigo imepewa kipaumbele kuliko mitandao mingine katika kuwaletea wateja wengi ladha mpya ya utumiaji waintaneti na mitandao ya kijamii kupitia lugha ya Kiswahili. Hii ndio maana halisi ya maisha ya kidigitali, pia inatimiza malengo yetu ya kuwashawishi wateja wengi zaidi wa Tigo kutumia data katika matumizi yao ya mawasiliano ya kila siku.”

Mkakati huu wa ushirikiano ni muendelezo wa mpango wa Facebook unaoitwa Internet.org uliozinduliwa na muasisi wa kampuni hiyo, Mark Zuckerberg.

Gutierrez alisema, “Huduma hii mpya itafungua milango mipya kwa Watanzania na watumiaji wengine wa Kiswahili kupata fursa za kibiashara, kielimu, na nyinginezo za kijamii na kiuchumi duniani kote.”

Ukiondoa nchi tano wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), Kenya, Tanzania, Uganda, Rwanda na Burundi, Kiswahili pia kina zungumzwa katika maeneo ya Malawi, Somalia, Zambia, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na Msumbiji.

Kwa uzinduzi huu, Tanzania taifa linayojulikana kama chimbulo la lugha ya Kiswahili, inayofahari ya kuwa nchi ya kwanza katika ukanda huu kutangaza lugha hii kimataifa, mafanikio ambayo hatuna budi yanatokana na ushirikiano kati yaTigo, kampuni mama ya Millicom na Facebook.

Hii ni mara ya pili kwa kampuni ya Facebook na Millicom kushirikiana katika kuzindua huduma ya Facebook kupitia simu bure ambapo Tigo nchini Paraguay walizindua huduma hii kwa mara ya kwanza Desemba 2013 katika lugha ya kiguarani inayotumika nchini humo.

Mkurugenzi wa Facebook wa Ushirikiano na Ukuaji wa Kimataifa Nicola D’Elia alisema, “Tunayo furaha kushirikiana na Tigo kwa mara nyingine tena kwa kuwapatia Watanzania wengi zaidi uwezo wa kuwasiliana kupitia utumiaji bure wa data katika app ya Facebook na tovuti ya simu, na sasa katika lugha ya Kiswahili.”
Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: