Jenerali Mark Milley, Kamanda wa Fort Hood akizungumza na waandishi wa habari
Wiki iliyopita, nchi ya Marekani ilikumbwa na mauaji mengine yaliyotokea kwenye kambi ya jeshi huko Fort Hood, Texas.

Jumatano Aprili 2, askari mmoja wa Jeshi la nchi hiyo, Ivan Lopez ambaye inasemekana alikuwa na matatizo ya msongo wa mawazo, aliwafyatulia risasi na kuwaua wanajeshi wenzake 3, kujeruhi 16 kabla hajajigeuzia bastola na kujiua

Mauaji haya, yanarejesha kumbukumbu ya mauaji makubwa kabisa kutokea kwenye kambi za jeshi nchini humo, yaliyotokea kwenye kambi hiyohiyo takriban miaka 5 iliyopita.
Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: