Tendega akizungumza na wanahabari 

Akizungumza na wanahabari nje ya iliyokuwa kambi ya Chadema mjini Iringa ya CK Lodge, Tendega alianza kwa kumshukuru Mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe na viongozi wengine wote walioshiriki kampeni za chama hicho. 

Huku baadhi ya wafuasi wa chama hicho wakiangua kilio alisema; “Ninawashukuru makamanda wenzangu na wanaharakati waliokuwa wanapigania haki Kalenga, wafuasi na wanachama wa Chadema wote, nawapa pole na hongera kwa kuanza na kumaliza uchaguzi huu uliokuwa na dosari nyingi,” alisema. 


Alisema maapambano ya ukombozi yana changamoto nyingi na kwamba huo ni mwanzo wa safari ya mabadiliko makubwa nchini, pale walipokesea mbele ya safari watajipanga upya. 
Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: