Mwenyekiti wa muda wa Morogoro Press
Club Boninveture Mtalimbo kulia akionekana katika picha tatu tofauti
akifafanua jambo wakati wa mkutano na waandishi wa habari juu ya
shughuli za uzindizi wa mfuko wa
jamii, uzinduzi wa Tovuti ya chama na bonanza la kukaribisha mwaka mpya
2013 na kuaga mwaka 2012 zinazotarajia kufanyika januari 19 mwaka huu
mkoani hapa. kushoto ni Mratibu wa miradi katika chama hicho Thadei
Hafigwa.
Mwandishi na mtangazaji wa IPP MEDIA mkoa wa Morogoro Idda Moshi kusho akichangia jambo katika mkutano huo na kulia ni Mratibu wa miradi katika chama hicho Thadei Hafigwa.
Mwandishi wa habari wa gazeti la
Mwananchi mkoa wa Morogoro Hamida Shariff kushoto akieleza jambo katika
mkutano huo, kulia ni Lilian Chuwa wa gazeti la Majira Morogoro.
Mwandishi Lilian
Chuwa wa gazeti la Majira Morogoro akifuatilia jambo na Lilian Lucas wa
Mwananchi wakati wa mkutano huo ambao ulihudhuriwa na waandishi
mbalimbali.
Mwandishi wa shirika la utangazaji la
TBCI mkoa wa Morogoro Monica Lyampawe akihoji jambo huku Mwandishi wa
IPP MEDIA Morogoro, Safia Maftaha akifuatilia matukio mbalimbali.
Na Thadei Hafigwa, Morogoro.
WAZIRI Mkuu Mstaafu Edward Lowasa anatarajiwa kuongoza shughuli za
uzindizi wa mfuko wa jamii pamoja na
Tovuti ya chama cha waandishi wa habari mkoa wa Morogoro (MOROPC) wakati wa
sherehe ya kuuaga mwaka 2012 na kuukaribisha 2013.
Hayo
yalibainishwa na Mwenyekiti wa Muda wa Moropc Boniventure Mtalimbo wakati
akiongea na waandishi wa habari kwenye ofisi za chama hicho, nakwamba uzinduzi
huo utafanyika Januari 19 mwaka huu katika hoteli ya kitalii ya Nashera mjini Morogoro.
Alisema lengo la kuanzishwa kwa mfuko wa
jamii ni kuwawezesha waandishi wahabari, kwenda vijijini kwaajili ya kuandika
habari kutokana na maeneo hayo kushindwa kufikika kwa urahisi kutokana na
ukosefu wafedha.
Mtalimbo
alisema mbali na waandishi kwenda vijijini pia utakuwa ukisaidia kwa mambo
mbalimbali ikiwemo kwenye maafa, kama vile vifo, magonjwa pamoja na kuwawezesha
kujiendeleza kielimu.
Akizungumzi uzinduzi wa tovuti (Website) alisema
waandishi wa habari mkoani Morogoro watakuwa wakiandika makala mbalimbali
zikiwemo za kuelimisha jamii,na kuandaa vipindi vya televisheni na redio na
kuingiza kwenye tovuti hiyo.
Aidha Mwenyekiti huyo aliwaomba wadau
mbalimbali ndani nanje ya mkoa wa Morogoro, kujitokeza kuchangiakwa hali na
mali mfuko huo ili kuwawezesha waandishi hao kufanya kazi kwa ufanisi zaidi
pamoja na kuibua mambo mbalimbali yaliyojificha hususani vijijini.
Aliwataja
wadhamini waliojitokeza hadi sasa kuwa ni Hoteli ya Nashera, Banki ya CRDB,
Mamlaka ya mapato Tanzania TRA,Kampuni ya Umeme ya Mac Dolnad Live line,Kampuni
ya Abood, Mbunge wa jimbo la Morogoro mjini Azizi
Abood, Mamlaka ya Maji safi na Taka mkoa wa Morogoro MORUWASA.


Toa Maoni Yako:
0 comments: