Serikali imeiagiza Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) kuhakikisha inajipanga kwa ajili ya kuboresha Viwanja vya Mwanza na Kilimanjaro ili kuweza kukabiliana na ongezeko kubwa la abiria watakaokuwa wakitumia Viwanja hivyo, baada ya Safari Za Ndege ya Fastjet kuanza.

Agizo hilo limetolewa leo na Naibu Waziri wa Uchukuzi, Dk. Charles Tizeba, wakati akiizundua Ndege ya Shirika la Ndege la Fast Jet jijini Dar es Salaam.

'Nawaagiza Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), kuhakikisha kuwa wanaviandaa Viwanja vya Mwanza na Kilimanjaro kwa ongezeko la Abiria ambao wanategemewa kutumia Viwanja hivyo. Ni matumani yangu Mamlaka inalichukua swala hili kwa umuhimu wake na itahakikisha kuwa hakuna Abiria atakaeshindwa kusafiri kwa sababu ya msongamano wa Abiria katika Viwanja Vyetu', Alisema Dk Tizeba.

Aidha Dk. Tizeba aliongeza kama sehemu ya jitihada za Serikali kuboresha Mazingira ya Sekta ya Usafiri wa Anga. Serikali imeweka mazingira mazuri kwa sekta binafsi kuwekeza katika ujenzi wa Miundombinu ya Viwanja Vya ndege.

"Serikali imeweka mazingira mazuri kwa sekta binafsi kuwekeza katika ujenzi wa Miundombinu ya Viwanja Vya ndege ambayo inakwenda sambamba mabadiliko ya sheria na maboresho ya kanuni'. alisema Dk. Tizeba.
 
Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la fastjet amesema siku ya leo ni siku muhimu sana si kwa Shirika hilo lakini pia na kwa Tanzania na Afrika maana usafiri wa bei rahisi umezunduliwa.

"Leo ni siku muhimu sana kwa Shirika la fastjet, Tanzania na Afrika kwa ujumla. Kwa Muda mrefu waafrika hawakuwa na usafiri wa Anga wa Uhakika na wa kuaminika .Fast jet itawawezesha kutumia usafiri wa Ndege na Shirika linatarajia kuwahakikishia usafiri wa bei nafuu kutoka sehemu moja kwenda nyingine'.alisema Bw. Edward.

Edward aliongeza mpaka saa Shirika limeshaajiri watanzania 70 ambapo miongoni mwao ni Wahudhumu wa Ndege(Vabin Crews), na watu wa masoko na akaongeza kuwa kampuni itaendelea kuajiri watanzania wengi kadri Shirika litakavyoongeza Ndege zake.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Mhandisi. Suleiman S. Suleiman amesema Mamlaka imejipanga kwa ajili ya kuboresha Sehemu za kusubiria Ndege na imeahidi kuendana na Mahitaji ya yanayotakiwa.
Shirika la Ndege la fastjet litaanza safari zake Tarehe 29 Novemba 2012 kwa safari mbili kila siku ambazo ni Kuanzia Dar es Salaam-Mwanza na Dar es Salaam-Kilimanjaro.Nauli  ya chini kabisa inakadiriwa kuwa Kiasi cha hilingi za kitanzania 32,000/- na Tiketi ya Juu kabisa inakadiriwa kuwa Shilingi za Kitanzania 92,000/- bei hizo zikiwa bila vat.

Lengo la Shirika hili ni kuvutia abiria wengi zaidi hasa wale wa kipato cha kawaida kuweza kutumia usafiri huo. Na kiwango cha Nauli ni kidogo ili kuwavutia wale ambao hawajawahi kutumia usafiri huo wautumie.
Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: