Mwanafunzi wa darasa la sita katika shule ya Msingi Malangali, iliyopo mkoani Iringa, Steven Mligo akitoa elimu kwa watoto wenzake juu ya Usalama barabarani na namna mbalimbali za matumizi sahihi ya barabara ikiwa ni pamoja na kutambua alama mbalimbali za barabarani. Mligo alikuwa akitoa elimu hiyo katika banda la Polisi Trafiki lililopo katika maonesho ya Wiki ya Nenda kwa Usalma Kitaifa inayofanyika Mkoani Iringa katika uwanja wa Samora chinbi ya Udhamini wa Kampuni ya simu ya Airtel.
Steven Mligo akitoa mafunzo kwa watoto wenzake na kuonesha dhahiri uwezo wake na jinsi alivyopata elimu hiyo ya usalama barabarani baada ya kupatiwa mafunzo shuleni kwao na maofisa wa Trafiki.
Mtaalam wa Elimu kutoka Mfuko wa Elimu Manispaa ya Iringa, Germana Kapinga (kulia) akimsikiliza mkazi wa mjini Iringa aliyetembelea banda lao lililopo katika maonesho ya Wiki ya nenda kwa Usalama viwanja vya Samora mjini Iringa leo.
Wakazi wa mjini Iringa wakimsikiliza, Mwenyekiti wa Taasisi ya Usalama barabarani watu wenye Ulemavu, Getram Kabate juu ya alama mpya kuu za makundi matano ya watu wenye ulemavu za usalama barabarani.
Kikosi kazi ambacho leo kilikuwa kikitoa elimu ya Usalama barabarani katika Maonesho ya maadhimisho ya Wiki ya Nenda kwa Usalama Barabarani mjini Iringa.
Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: