*Dk.
Bana asema harakati zao hazikubaliki
*Tendwa naye awatega
kuhusu ruzuku
Na Mwandishi Wetu
CHAMA
Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimetupiwa lawama kwamba harakati zake
za kisiasa zinatishia usalama na amani ya nchi.
Hayo
yalijitokeza jijini Dar es Salaam leo, katika Kongamano liliitishwa na Msajili
wa Vyama vya Siasa nchini John Tendwa na kuwashirikishaviongizi wa vyama vyote
vya siasa.
Kongamano
hilo lilikuwa likijadili umuhimu wa amani na usalama wa nchi, wajibu wa Jeshi
la Polisi na vyama vya siasa katika kukuza demokrasia ya vyama vingi.
Baadhi
ya wadau na vyama kutoka vyama mbalimbali vya siasa nchini walikitupia lawama chama
hicho na kudai kuwa kimekuwa mstari wa mbele katika kuvunja sheria na maadili
ya taifa.
Mhadhiri
Mwandamizi wa Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam, Dk. Benson Bana, alisema harakati
zinazoendeshwa na CHADEMA, hazikubaliki na zinalenga kuvunja sheria za nchi.
Dk.
Bana, alisema alikosoa kile harakati za chama hicho kupitia oparesheni yake ya Vuguvugu
la Mabadiliko (M4C), kwa kufanya mikutano kila kona ya nchi haina tafsiri nyingine yoyote zaidi ya kutaka
kuvunja amani na usalama wa nchi.
Katika
mada yake, iliyohusu, Mazingira wezeshi na hatarishi katika kujenga na kukuza
mfumo wa vyama vingi vya siasa, Dk. Bana, alisema, CHADEMA, ni chama kikubwa na
chenye nguvu kuweza kuchukua dola, hivyo kinapaswa kuonyeshwa mfano kwa umma hasa
katika kutii na kuheshimu sheria.
Alisema
mikutano na maandamano ya CHADEMA
yanayofanyika kila mahali nchini hayana lengo zuri kwa sababu muda huu si
wakati wa kampeni za uchaguzi.
Mharidhi
huyo wa siasa ambaye pia ni Mwenyekiti wa REDET, alisema kinachofanywa sasa na chama
hicho si kueneza sera zake bali ni sawa na kampeni za uchaguzi kabla ya muda
wake.
Alisema
wakati huu ni wakati wa vyama vya siasa kujijenga kwa kufanya mikutano ya ndani
ya chama, kuandaa viongozi kwa ajili ya uchaguzi wa serikali za mitaa, uchaguzi
mkuu 2015 pamoja na kuhamasisha wananchi washiriki shughuli za maendeleo na si
kufanya mikutano na maandamano yanayofanana na kampeni za uchaguzi.
Alisema,
kauli mbiu ya M4C, ni nzuri lakini haifai kwa wakati huu, na kusema ikitokea kila chama
cha siasa kilichopata usajili kutaka kufanya siasa kwa maandamano na mikutano kama
CHADEMA nchi haitatawalika.
Dk.
Bana, pia alizungumzia hatua ya CHADEMA kususia kongamano hilo, huku akisema si
hatua nzuri kwani inaonyesha chama hicho hakina uvumilivu wa kisiasa.
“CHADEMA
ni chama kikubwa ambacho kimejijengea heshima kubwa na kinatarajiwa kuchukua
dola wakati wowote, kwa hiyo hakina budi kufuata na kuzingatia sheria za nchi
ili kuonyesha mfano kwamba kipo tayari kuongoza umma.
“Mimi
sielewi hizi harakati zao zinalenga nini, sioni umuhimu wake, vyama vya siasa baada
ya uchaguzi huwa vinapata muda wa kujitathimini na kufanya mikutano ya ndani
siyo vuguvugu, lakini kinachofanywa na CHADEAMA sasa ni kampeni za uchaguzi
ambazo si wakati wake,
“Hii
si nchi ya mabadiliko, tunayo serikali iliyowekwa madarakani na wananchi kwa
mujibu wa sheria, sasa wanaandamana kupinga nini? Alisema na kuhoji Dk. Bana
“Wakiendelea
namna hii, nchi itapelekwa pabaya, haya maandamano na vuguvugu hizi zinaweza
kuhatarisha amani na usalama wa nchi, hakuna uhuru,
Tendwa naye anena
Msajili
wa vyama vya siasa, John Tendwa, alisema kitendo cha CHADEMA kususia kongamano
hilo siyo cha kiungwana.
Alisema,
kongamano hilo, lilikuwa na nia njema ya kuwaweka karibu viongozi wa jeshi la
Polisi, vyama vya siasa pamoja na ofisi yake ili kutafuta muafaka wa kitaifa.
Toa Maoni Yako:
0 comments: