Siku  moja mara baada ya majambazi kuvamia gari ya abiria aina Land Cruser yenye namba za usajili T 853 BLF na kujeruhi watu sita na mtu kufariki, Jeshi  la  polisi mkoani Rukwa limeanza kuwasaka watu hao katika milima ya Muze na vijiji jirani  yanakodhaniwa  kukimbilia majambazi  hayo huku wananchi wakitakiwa  kutoa  taarifa pindi watakapopatikana.

Oparesheni hiyo inayoongozwa na kamanda wa polisi  mkoa  wa Rukwa Isuto Matage imeanzia eneo ambalo waliteka  gari hilo na kuendelea katika vijiji vya bonde  la ziwa Rukwa nyumba kwa nyumba ili kuwabaini majambazi hao.

Katika vijiji  vya Mwale na mto wisa Kamanda Isuto anakutana na vikundi vya vijan  na wanachi  ili  kutoa elimu ya ulinzi shirikishi ikiwa ni moja ya mbinu ya kuwapata majambazi  hao wanaosadikiwa kutoka nchi jirani.
Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: