BARNABA JINA: Elias Barnabas
TAREHE YA KUZALIWA: 08/08/1990
MAHALI ALIPOZALIWA: Morogoro.

ELIMU YAKE;

1998-2004 elimu ya msingi Kinondoni shule ya msingi.
2005-2007 elimu ya sekondari aliishia kidato cha tatu.

ALBAMU YAKE;

Albamu yake ya kwanza aliifanya kwa kipindi cha kati ya 2008-2010 kwa ushirikiano na Amini iliyotambulika kwa jina la Njia Panda ambayo ilikuwa na jumla ya nyimbo 14 ambapo baadhi ya nyimbo zinazopatikana katika albamu hiyo ni pamoja na:

Njia panda: .iliyoimbwa naye Barnabas pamoja na Pipi
Muongo’ ,Robo saa, na Mbala mwezi zote zimeimbwa na Amini pamoja na Barnabas.
Wrong Number, iliyoimbwa na Barnabas pamoja na Linah

MAISHA YAKE KABLA YA MUZIKI

Baada ya kukatiza elimu yake ya sekondari alikuwa akitumia muda wake mwingi kuuza genge la vyakula lililokuwa nyumbani kwao pamoja na kupiga vyombo mbalimbali vya muziki katika kanisa lao ambapo alipendelea sana kupiga Drums na gita.

KUHUSU FAMILIA YAKE

Familia anayotokea Barnaba ina jumla ya watoto watatu wakati Barnaba akiwa ni mtoto wa kwanza kuzaliwa kutoka kwenye familia ya Mzee Barnabas.

MAISHA YAKE BINAFSI

Barnabas bado anaishi nyumbani kwao maeneo ya kigogo ambapo anaishi na familia yake.

Barnabas anamiliki duka linalouza vyakula lililopo maeneo ya Kinondoni .
Kila mwisho wa juma Barnabas huwa anapendelea kutembelea katika ufukwe wa bahari.
FALLY IPUPA ALIMSHAWISHI KUIMBA.

Barnabas alishawishiwa sana na msanii wa bolingo kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) FallyIpupa , kuimba muziki kutokana na kuwa ni mwanamuziki pekee wa anayemvutia barani Afrika..

MBALI NA MUZIKI;

Mbali na muziki Barnabas anajihusisha pia na shughuli za biashara za uuzaji wa vyakula kwenye duka lake lililopo maeneo ya Kinondoni.

KWA MUDA GANI AMEKUWA AKIIMBA?

Barnabas amekuwa akiimba kwa muda wa miaka minne sasa tangu alipojiunga rasmi na T.H.T mwaka 2006 baada ya kupelekwa na rafiki wake wa karibu aliyekuwa anasali naye kanisani.

MIPANGO YA BAADAE YA BARNABAS KIMUZIKI

Mpango mkubwa na wa kwanza wa Barnabas ni kurudi shule, na hii ni kutokana na ukweli kuwa yeye hakuweza kubahatika kuendelea na masomo hadi ngazi ya juu ya kielimu.

SIKILIZA SONGI LAKE JIPYA ANALOTAMBA NALO KWA SASA... Linaitwa Milele Daima.
Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: