JK akimnadi mgombea ubunge jimbo la Isimani ambaye kapita baada ya kukosa mpinzani Mh. William Lukuvi huko Isimani leo
JK akiondoka Isimani baada ya kuhutubia mkutano mkubwa wa kampeni
JK akihutubia wananchi wa Isimani
Wasanii wa Tip Top Family na TMK family walikuwepo Isimani leo
Mgombea ubunge Iringa Mjini Mh. Monica Mbega akikumbatiana kwa furaha na Frederick Mwakalebela ambaye alikuwa mpinzani wake kwenye kura za maoni
Mwanasiasa mkongwe Mh. Paul Kimiti akiwa na mgombea Ubunge Iringa mjini na Frederick Mwakalebela uwanja wa Samora mjini Iringa leo. Wahasimu hao katika kura za maoni walitangaza kuvunja makundi na kumpigia upatu mama Mbega pamoja na wagombea udiwani
Pamoja na kutopitishwa katika kura za maoni Frederick Mwakalebela na wagombea wengine wa ubunge na udiwani Iringa mjini walikuwepo uwanja wa Samora kukiunga mkono CCM
Sehemu ya umati uliojitokeza Uwanja wa Samora leo kumsikiliza JK akimwaga sera
Wageni wa mataifa mbalimbali walikuwepo pia
Nyomi uwanja wa Samora
Uwanja wa Samora ulifurika
Wananchi kibao wa Iringa walijitokeza wananchi wa Iringa wakimsikiliza JK uwanja wa SamoraJK akiwasili katika kijiji cha Kilolo tayari kwa kufanya mkutano wa kampeni
JK akiwa na aliyekuwa mgombea ubunge wa Iringa mjini Bw. Frederick Mwakalebela kwa pamoja wakiwasalimia wananchi waliofika kwenye mkutano wa kampeni za chama hicho uliofanyika katika uwanja wa Samora mkoani Iringa. Mwakalebela, huku akishangiliwa na maelfu ya wakazi wa mji huo, aliweka historia ya kuwa mwana CCM aliyenadiwa hadharani pamoja na kushindwa katika kura za maoni ambapo alipopanda jukwaani sio tu alitangaza kuvunja makundi bali pia kuomba wananchi wa Iringa kumpa kura mshindani wake Mh. Monica Mbega na madiwani pamoja na Rais kwenye uchaguzi mkuu Octoba 31.

JK akikumbatiana na Mwakalebela leo uwanja wa samora
Mgombea Urais chama cha CCMMh Jakaya Kikwete na Frederick Mwakalebela.
Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: