Wanachama wa Urambo wakiwa na mabango wakati wakimpokea Mgombea Mwenza wa urais kupitia tiketi ya CCM, Dk. Mohamed Gharib Bilal, alipokuwa akiwasili kwenye Viwanja vya Ofisi za Spika kufanya mkutano wa kampeni na kumnadi mgombea ubunge wa jimbo la Urambo Mashariki, Samuel Sitta leo Septemba 21 2010.
Mgombea Mwenza wa urais kupitia tiketi ya CCM, Dk. Mohamed Gharib Bilal, akisalimiana na Mgombea Ubunge wa Jimbo la Urambo Mashariki, Samuel Sitta, wakati alipokuwa akipokelewa mpakanani mwa Wilaya ya Uyui na Urambo leo.
Dk. Mohamed Gharib Bilal, akisalimiana na Mbunge wa Viti Maalu wa Mkoa wa Tabora Mama Samuel Sitta, wakati alipokuwa akipokelewa mpakanani mwa Wilaya ya Uyui na Urambo leo .
Mgombea Mwenza wa urais kupitia tiketi ya CCM Dk. Mohamed Gharib Bilal, akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Usoke baada ya kusimama kuwasalimia wananchi wa kijiji hicho alipokuwa akipokelewa kuingia Wilaya ya Urambo kufanya mkutano wa kampeni katika Jimbo la Urambo Mashariki katika Jimbo la Samuel Sitta leo.



Toa Maoni Yako:
0 comments: