Kundi la Original Comedy wakiwa katika Studio za TBC1 wakati wa mazoezi ya onesho lao ambalo limepokelewa kwa shangwe na washabiki wao toka warudi hewani wiki mbili zilizopita. Hivi sasa hakuna anayetumia jina lake alilokuwa anatumia EATV bali sasa wana No-Name 1 hadi 7.

Kesho Original Comedy wanafanya onesho lao la kwanza la wazi katika ukumbi wa Diamond Jubilee.

Kipindi cha kwanza cha kundi hilo kilirushwa na televisheni ya taifa TBC1 huku kikionyesha kuwa ni moto wa kuotea mbali kwa kulikuwa na vituko vya aina mbalimbali.

Kundi hilo limekuja na sura mpya baada ya majina yote ya wasani hao kubadiliwa huku na jina lakipindi chenyewe likibadilika kutoka ze Comedy hadi Comedy Original.

Baadhi ya washabiki wa kipindi hicho wameelezea kufurahishwa kwao na kurejea kwa maonyesho ya kundi hilo na kusema afadhali watapata muda wa kufurahisha pindi wanapokuwa majumbani kwao.
Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: