Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Kassim Majaliwa Kassim akizindua Wiki ya Vijana kitaifa uliofanyika Jijini Mwanza.


Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Mungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Kassim   amewataka vijana wa Kitanzania kutumia fursa za maendeleo ya kidigitali kama njia ya kujitengenezea fursa za ajira na kuacha kutumia mitandao ya kijamii kwa mambo yasiyofaa.

Mhe. Majaliwa amewataka vijana kufichua na kuziainisha taasisi zenye nia ovu ya kuharibu na kuvunja mila na desturi za Kitanzania, pamoja na taasisi hizo binafsi kujitambulisha na kutoa malengo ya Taasisi.

Katika kuadhimisha siku ya Vijana Kitaifa, Shirika lisilo la kiserikali la BRAC Maendeleo Tanzania,limeadhimia kuendelea na kuwekeza kwenye kutoa elimu zaidi kuhusiana na maendeleo ya vijana

Akizungumzia maadhimisho hayo, Meneja wa Mkoa Mwanza Novatus Tarimo amesema elimu wanayotoa kwa vijanai ni  kuwawezesha vijana kupaza sauti kwa Serikali na  jamii ili waweze kujiinua kiuchumi kupitia fursa mbalimbali zilizopo.

Amesema, Shirika la BRAC Maendeleo Tanzania limekuwa na miradi ya uwezeshaji kiuchumi kwa vijana na ikiwa ni katika  kuunga mkono Serikali ya awamu ya sita kwa kuwainua kiuchumi na kuwapa fursa za kujiajiri.

Tarimo amesema,  wao ni Wadau namba moja wa maendeleo na wamekuwa wakifanya kazi na Serikali kwa ngazi ya kitaifa na  kuwekeza kwenye kutoa hamasa kutokana na matakwa muhimu kwa wakati huo.

 "Vijana ndio taifa la kesho, kuna kila sababu ya kuwasaidia vijana hawa kwa kupaza sauti zao na kuwapatia elimu ya zaidi ili waweza kujiendeleza na kujiinua kiuchumi na kujiajiri,"amesema Tarimo.

"Mradi wa AIM, unaojihusisha na utoaji wa elimu na uwezeshaji wa kiuchumi na katika kipindi chote umekuwa na mafanikio makubwa sana,"

BRAC Maendeleo ni shirika lililojikita katika kuwezesha kiuchumi vijana kwa elimu ya ujasiriamali, na kwa kutoa mikopo ya vikundi kwa wakina.mama kupitia BRAC Finance Limited.

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Kassim aizungumza na Vijana waliojitokeza katika viwanja hivyo  amewataka vijana wa Kitanzania kutumia fursa za maendeleo ya kidigitali kama njia ya kujitengenezea fursa za ajira na kuacha kutumia mitandao ya kijamii kwa mambo yasiyofaa.Maandamano ya wafanyakazi na vijana wa BRAC Maendeleo Tanzania wakati wa maadhimisho ya Wiki ya Vijana Kitaifa yaliyofanyika Jijini Mwanza.
Wananchi wakipita na kupata maelezo kutoka wafanyakazi wa BRAC Maendeleo Tanzania kuhusiana na uwezeshaji wa Vijana nchini
Next
This is the most recent post.
Previous
Older Post
Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: