Mke wa Makamu wa Raisi Zakia Bilali akiwasha jiko la gesi ikiwa ni ishara ya uzinduzi wa mtambo wa gesi inayo tokana na kenyesi cha ng’ombe ambayo imetengenezwa na washiriki wa maisha plus kulia kwake ni mlezi wa chama cha wake wa viongozi (New Mellinium Women Group) Mke wa Waziri Mkuu Mama Tunu Pinda wakiwa na wake viongozi wakishuhudia uzinduzi huo ambao umefanyika katika kambi ya Maisha Plus iliyopo wilayani Bagamoyo Pwani. Picha na Chris Mfinanga.
 Mlezi wa chama cha wake wa viongozi (New Mellinium Women Group) Mama Tunu Pinda akiwongoza wakina mama wenzake kuelekea katika kambi ya Maisha Plus aliye nyuma yake ni Mke wa Makamu wa Raisi Zakia Bilali. Wakina mama hao walifika katika kambi hiyo ili kujionea shughul zinazo fanywa na washiriki katika maisha Plus iliyopo Bagamoyo Pwani.
 Mke wa Makamu wa Raisi Zakia Bilali akiwa na Mlezi wa chama cha wake wa viongozi New Mellinium Women Group Mama Tunu Pinda pamoja na Katibu wa chama hicho cha wake wa viongozi Mama Pamela Mathayo wakiangalia shamba la mfano ambalo washiriki wa maisha Plus wanaliandaa.
Wanachama wa cha Wake wa Viongozi New Mellinium Women Group wakiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa Maisha Plus wa hapa nchini na nnje ya nchi pamoja nawaandaji. Picha na Chris Mfinanga
Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: