Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete wakwanza kushoto akiwa na Waziri wa Ujenzi Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt. Rehema Nchimbi pamoja na Mbunge wa Kongwa ambaye pia ni Naibu Spika Job Ndugai wakifurahia mara baada ya Rais kuweka jiwe la Msingi Ujenzi wa Barabara ya Mbande-Kongwa 16.5Km .
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na Waziri wa Ujenzi Dkt. John Pombe Magufuli, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt. Rehema Nchimbi, Mbunge wa Kongwa ambaye pia ni Naibu Spika Job Ndugai, Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Miundombinu Profesa Juma Kapuya pamoja na Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi Mhandisi Mussa Iyombe, akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa barabara ya Mbande-Kongwa 16.5Km.
Waziri wa Ujenzi Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akipiga ngoma pamoja na kikundi cha ngoma za asili cha Kibaigwa kabla ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete kuhutubia mamia ya Wakazi wa Kibaigwa.
Sehemu ya barabara Mbande-Kongwa 16.5Km ambayo ujenzi wake umewekwa jiwe la Msingi.
Waziri wa Ujenzi Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli kulia akizungumza na Mbunge wa Kibakwe ambaye pia ni Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mheshimiwa George Simbachawene huku Mbunge wa Kongwa ambaye pia ni Naibu Spika Job Ndugai akishuhudia kushoto.
Waziri wa Ujenzi Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli katikati akizungumza na Mbunge wa Kongwa ambaye pia ni Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Job Ndugai (kushoto) pamoja na Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Miundombinu Profesa Juma Kapuya(kulia) kabla ya uzinduzi wa barabara ya Mbande-Kongwa 16.5Km.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza na Waziri wa Ujenzi Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli mara baada ya uzinduzi na ufunguzi wa barabara ya Mbande-Kongwa 16.5Km
Viongozi mbalimbali kutoka Wizara ya Ujenzi pamoja na Taasisi zake wakimsubiri Rais Dkt. Jakaya Kikwete kuzindua rasmi mradi wa Ujenzi wa Barabara ya Mbande-Kongwa 16.5Km.  Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Ujenzi
MWENYEKITI wa Bunge Maalum la Katiba, Mhe. Samuel Sitta (pichani juu) amevitaka vyombo vya habari nchini kuacha uchochezi na chuki wakati vinapohabarisha umma kuhusiana na mchakato wa Katiba Mpya.

Kauli hiyo nimetolewa leo na Mhe. Sitta wakati alipokutana na baadhi ya waandishi wa habari katika viwanja vya Bunge mjini Dodoma huku akiviasa vyombo vya habari kuachana na kuandika habari zenye kuleta uchochezi na  chuki ili kuvuruga mchakato wa Katiba Mpya.

Mhe. Sitta amesema kuwa kuna baadhi ya watu wamekuwa na dhana tofauti kuhusu kazi ifanywayo na  Bunge Maalum la Katiba, hivyo ni vema kuepukana nao na kuhabarisha umma taarifa sahihi ili Katiba Mpya iweze kupatikana.

”Kusema tunafanya kazi ya Tume ni upotoshaji mkubwa, sisi tunafanya kazi tuliyotumwa tena kwa uadilifu mkubwa.upotoshwaji mwingine  unafanywa na baadhi ya watu ambao hawalitakii mema Taifa letu na hawapendi kuona mchakato wa Bunge la Katiba unaendelea vizuri,” alisema Mhe. Sitta.

Mhe. Sitta ameongeza kwa kutolea ufafanuzi juu ya baadhi ya makundi yaliyowasilisha mapendekezo yao katika Bunge hilo, kwa kusema kuwa maoni yanayoletwa na makundi mbalimbali kwa lengo la kuboresha Rasimu Mpya ya Katiba yanapokelewa lakini sio maoni tu ya mtu binafsi au mwananchi, bali wanapokea maoni kupitia makundi maalum kama yalivyo kwa wafugaji, Wasanii na Wakulima ambao wameshawahi kuwasilisha maoni na mapendekezo yao  katika iliyokuwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba lakini hayakuonekana na mengine yalisahaulika  katika Rasimu hiyo. 

“Tuna haki na wajibu wa kuyapokea makundi haya ili kutoa Katiba iliyo rafiki kwa wananchi wote,” alisisitiza Mhe. Sitta.

Wakati huohuo, baadhi ya Wenyeviti wa Kamati mbalimbali za Bunge hilo, wamesema wamemaliza kazi ya kuchambua Rasimu hiyo vizuri katika Kamati zao.

Akizungumzia kuhusu kazi hiyo, Mwenyekiti wa Kamati Namba Tatu ya Bunge hilo, Dkt. Francis Michael amesema suala  la ardhi lilionekana kuwa nyeti katika Kamati yake.

Dkt. Francis aliongeza  kuwa suala la kupokea mapendekezo kutoka kwa makundi mbalimbali si kwamba kila kitu kitawekwa kwenye  Katiba Mpya bali  ni yale mambo ya msingi.

Naye Mwenyekiti wa Kamati Namba Moja ya Bunge hilo, Mhe. Ummy  Mwalimu Ally na Makamu Mwenyekiti wa Kamati Namba Kumi na Moja, Mhe. Hamad Massauni walisema kuwa katika Kamati zao majadiliano yalikwenda vizuri.
 Rais Jakaya Kikwete  wa Tanzania (kulia) na Rais Pierre Nkurunzinza wa Burundi (kushoto) wakishikana mikono ikiwa ni ishara ya kudumisha umoja na mshikamano mara baada ya kuzindua  alama ya mpaka inayotenganisha nchi za Tanzania na Burundi.
---
Na Aron Msigwa – MAELEZO - Ngara, Kagera.

Marais wa Tanzania na Burundi wamewatoa hofu wakazi wa maeneo ya mpakani mwa Tanzania na Burundi kuwa zoezi Uimarishaji wa mpaka wa kimataifa kati ya nchi hizo linalofanywa na wataalam wa upimaji na ramani katika maeneo ya mipaka ya nchi hizo halilengi kuleta mgawanyiko miongoni mwao bali kuweka utaratibu mzuri wa utambuzi wa alama za mipaka ya kimataifa na kuwawezesha wananchi wa pande zote kuwa na uhakika wa uhalali wa maeneo wanayoishi.


Wakizungumza kwa nyakati tofauti na wananchi wa kijiji cha Mugikomero wilayani Ngara kwa upande wa Tanzania na Nteritare kwa upande wa Burundi wakati wa uzinduzi wa zoezi uimarishaji wa mpaka kati ya Tanzania na Burundi viongozi hao wamesema kuwa Serikali za nchi zote zimeamua kufanya zoezi hilo kufuatia mabadiliko mbalimbali yaliyojitokeza katika maeneo ya mipaka ikiwemo alama za kwanza zilizowekwa na wakoloni mwaka 1924 kuchakaa na nyingine kung’olewa na wananchi kutokana na sababu mbalimbali, ongezeko la watu, shughuli za kiuchumi na baadhi ya maeneo ya mito iliyokuwa ikitenganisha nchi hizo kukauka.

Rais wa Tanzania Mh. Dkt. Jakaya Kikwete akizungumza na wananchi wa vijiji hivyo amesema kuwa kufanyika kwa zoezi hilo kunatokana na agizo la Umoja wa Nchi za Afrika (AU) lilotolewa mwezi June 2007 katika kikao cha wakuu wa nchini za Afrika kilichofanyika Accra, Ghana ambacho kilizitaka nchi zote za Afrika kuhuisha upya mipaka ifikapo mwaka 2017 ili kuondoa migogoro ya mipaka inayojitokeza.

Amesema baadhi ya nchi za Afrika zimekuwa katika malumbano na machafuko ya mipaka kutokana na kutokuwa makini katika kuhakiki maeneo ya mipaka na kuongeza kuwa Serikali ya Tanzania itahakikisha kuwa zoezi hilo linaendeshwa kwa ufanisi mkubwa katika maeneo mengine yaliyobaki.

“ Sisi na Burundi ni ndugu wa damu tumechagua njia ya mazungumzo na kalamu, Marafiki huchora mipaka kwa mazungumzo na kalamu, maadui huchora mipaka kwa nguvu na kwa wino wa damu, mipaka ya kalamu hudumu na hustawisha jamii wakati ile ya damu huleta chuki, hujuma ,dhuluma na kisasi” Amesisitiza.

Amesema kuwa serikali ya Tanzania kwa kushirikiana na Serikali ya Burundi itahakikisha kuwa eneo lote la mpaka kati ya Tanzania na Burundi lenye urefu wa kilometa 450 katika mikoa ya Kagera na Kigoma linafikiwa licha ya kuwepo kwa changamoto mbalimbali na gharama kubwa za kufanikisha zoezi hilo.

“Maeneo mengi yako msituni, yako kwenye mabonde, mito na ni vigumu kuyafikia,tumeamua kuyagharamia na kufanya wenyewe kwa fedha zetu wenyewe kuonyesha dhamira na utashi wetu kulikamilisha zoezi hilo kabla ya muda uliowekwa ili kuondoa sintofahamu iliyokuwepo” Amesisitiza.

Amesema kuwa serikali itahakikisha kuwa inatenga fedha za kutosha kukamilisha zoezi la uwekaji wa alama za mipaka ili kuwezesha serikali za nchi mbili kuwa na mkataba mpya ambao utafuta mkataba uliowekwa na wakoloni.

Amewataka wakazi wa maeneo hayo kuwa walinzi wa alama za mipaka na kuepuka kuhujumu zoezi hilo, kulima katika maeneo ya hifadhi kutokana na umuhimu wa alama hizo kimataifa na kwa wakazi wa maeneo husika kwa kuwa zoezi hilo baada ya kukamilika litaondoa mashaka kuhusu uhalali wa maeneo wanayoyamiliki, huduma, shughuli za biashara na ujenzi wa makazi.

Kwa upande wake Rais wa Burundi Mh. Pierre Nakurunzinza ameishukuru Serikali ya Tanzania kwa kuendelea kushirikiana na serikali ya Burundi katika kutekeleza majukumu na masuala mbalimbali yenye manufaa kwa wananchi.

Amesema ushirikiano katika zoezi hilo unaonyesha wazi kuwa Serikali za nchi zote mbili zinafanya kazi kwa ushirikiano mkubwa na kuongeza kuwa kuanza kwa zoezi hilo ni uthibitisho tosha kuwa waafrika wanaweza kufanya mambo yao wenyewe kwa ufanisi mkubwa.

Amefafanua kuwa Tanzania imefanya mambo mengi sana kwa serikali ya Burundi na hilo linathibitisha dhamira safi na ushirikiano mkubwa tokea wakati wa machafuko na vita iliyotokea nchini Burundi.

“Serikali ya Tanzania imekuwa bega kwa bega na serikali yetu ya burundi,Tanzania imefanya mambo mengi sana kwa wananchi wa Burundi, iliwahifadhi wananchi wa Burundi wakati wa machafuko,iliwalisha iliwatunza na kuwathamini na zoezi tunalolifanya sasa la kuhakiki mipaka ni dogo sana ikilinganishwa na undugu na umoja wetu” Amesisitiza.

Amewataka wakazi wa pande zote mbili kuhakikisha kuwa wanatoa ushirikiano kwa wataalamu wa upimaji na ramani wa nchi zote mbili na kuongeza kuwa wananchi wote watakaoathiriwa na zoezi hilo kutokana na kupoteza maeneo yao watalipwa fidia na kutafutiwa maeneo mengine.

Kwa upande wao mawaziri wa Ardhi,Nyumba na Makazi wa nchi hizo Prof. Anna Tibaijuka wa Tanzania na Jean Claude Nduwayo wa Burundi wameeleza kuwa zoezi la uhakiki wa mpaka wenye urefu wa kilometa 450 na alama 58 zilizoanzia Pwani ya Mashariki ya Ziwa Tanganyika hadi Kusini mashariki mwa mto Mwibu lina manufaa makubwa kwa wananchi wan chi zote mbili.

Wamesema Tanzania na Burundi zimefanya kazi kwa ushirikiano kupitia kamati ya Pamoja ya Ufundi ya Mipaka ya Kimataifa (JTC) amabayo ilitoa maamuzi muhimu ya ufanikishaji wa zoezi hilo ikiwemo uamuzi wa upana wa eneo la wazi la mpakani (buffer zone) kuwa mita 12.5 kila upande wa mpaka, Kuanza kwa kazi ya uimarishaji wa mpaka mwezi Machi mwaka huu pamoja na uratibu wa shughuli ya uzinduzi wa shughuli ya uimarishaji wa mipaka.

Wamefafanua kuwa uamuzi wa kuimarisha mpaka umetokana na kuwepo kwa ongezeko kubwa la shughuli za kiuchumi katika maeneo ya mpakani, hali ya mabonde na milima iliyopo ya mabonde na milima katika sehemu kubwa ya mipaka inayofanya utambuzi wa mpaka kuwa mgumu kwa wananchi wa kawaida.
Peroni Nastro Azzuro inakuletea Fashion Night Out na Rio Paul. Kwa mara ya kwanza kabisa zitatambulishwa kazi za mbunifu mavazi Rio Paul. Njoo ufurahie usiku uliopambwa na mitindo, muziki toka kwa HtheDJ na pati isiyosahaulika ndani ya News Cafe.
Mhariri Mkuu Msaidizi wa Jarida ya Euromoney bwana; Duncan Kerr (kulia) na Mkurugenzi Mkuu wa NMB Mark Wiessing (katikati) akipokea chti cha benki bora, kushoto ni mtendaji mkuu wa ukagusi wa ndani wa NMB Augustino Mbogella

Na Mwandishi Wetu.

Jarida la kimataifa la Euromoney la Uingereza limeitaja NMB kuwa benki bora Zaidi kwa mwaka 2014 katika hafla ya utoaji wa tuzo hizo iliyofanyika jijini London hivi karibuni. Hii ni mara ya pili mfululizo kwa NMB kutajwa kama benki bora Tanzania ambapo mwaka 2013 pia NMB iliibuka kidedea na kutajwa benki bora Tanzania-2013.

Kila Mwaka, Jarida la Euromoney huandaa hafla ya kuyatambua Zaidi ya Makundi 20 ya bidhaa za kitaasisi za kifedha zikiwemo benki kote duniani kwa kuagalia benki bora na ya kiwango cha juu kwa kila bara na benki bora katika nchi takribani 100 duniani kote. Tuzo hii huzitambua taasisi za kifedha duniani kote ambazo zimepata mafanikio ya hali ya juu katika maeneo yao, kwa kuonyesha ugunduzi na kupata mafanikio ya kifedha kila mwaka.

Jopo la wataalam kutoka mataifa mbalimbali na wenye utaalamu mbalimbali hupitia taarifa zinazowasilishwa na taasisi zote za kifedha duniani na kutangaza washindi.

Ndani ya miezi 12, benki ya NMB imeanzisha huduma mbali mbali za kibenki na hivyo kuendelea kuwafikia wateja wa huduma za kibenki kuanzia kuweka akiba, kutoa na kuchukua fedha mijini na vijijini. Kama benki ya kitanzania yenye wateja Zaidi ya milioni 2, Mpango wa NMB unadhihirisha dhamira yake kuhusu elimu juu ya masuala ya kifedha kwa watanzania.” Alisema Mark Wiessing.

“Tunatoa shukrani zetu wa wateja, wafanyakazi na washika dau wote kwa kuwa sehemu ya mafanikio haya makubwa kwa benk, “ alisema Wiessing na kuongeza kuwa NMB itaendelea na ahadi yake ya kuwapa huduma bora wateja wake sasa na siku za mbeleni.

Wiessing aliongeza pia kuwa tuzo hiyo inaongeza kwenye hazina ya tuzo ambazo benki imezipata katika miezi 12 huku akizitaja baadhi kuwa ni benki bora ya mwaka kutoka jarida la Banker, Mamlaka ya mapato Tanzania (TRA) wakiipa NMB tuzo ya mlipakodi anaefuata sharia katika taasisi za kifedha nchini. Mwaka 2013 jarida la Euromoney pia liliitaja benki kuwa Benki bora Tanzania huku taasisi ya Super Brand ya Kenya ikiitaja benki bora Tanzania katika taasisi 20 bora Tanzania kwa 2013/3014 na Jarida la the Banker pia liliitaja NMB kuwa benki bora ya kibiashara Afrika Mashariki.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Rais Pierre Nkurunzinza wa Burundi alipowasili eneo la mpaka kati ya Tanzania na Burundi la Mugikomero wilayani Ngara mkoani Kagera kwa upande wa Tanzania na eneo la Nteritare kwa upande wa Burundi wakati wa sherehe za uzinduzi wa programu ya uimarishaji wa mipaka ya kimataifa Jumatano Agosti 27, 2014.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na Rais Pierre Nkurunzinza wa Burundi baada ya kuwasili eneo la mpaka kati ya Tanzania na Burundi la Mugikomero wilayani Ngara mkoani Kagera kwa upande wa Tanzania na eneo la Nteritare kwa upande wa Burundi kuhudhuria sherehe za uzinduzi wa programu ya uimarishaji wa mipaka ya kimataifa Jumatano Agosti 27, 2014.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na Rais Pierre Nkurunzinza wa Burundi baada ya kuwasili eneo la mpaka kati ya Tanzania na Burundi la Mugikomero wilayani Ngara mkoani Kagera kwa upande wa Tanzania na eneo la Nteritare kwa upande wa Burundi kuhudhuria sherehe za uzinduzi wa programu ya uimarishaji wa mipaka ya kimataifa Jumatano Agosti 27, 2014. Wengine ni Waziri wa Ardhi na Maendeleo na Makazi, Profesa Anna Tibaijuka na Balozi wa Burundi nchini Tanzania Mhe Issa Ntambuka.
Rais Pierre Nkurunzinza wa Burundi akisalimiana na Waziri wa Nishati na Madini wa Tanzania Profesa Sospeter Muhongo eneo la mpaka kati ya Tanzania na Burundi la Mugikomero wilayani Ngara mkoani Kagera kwa upande wa Tanzania na eneo la Nteritare kwa upande wa Burundi kuhudhuria sherehe za uzinduzi wa programu ya uimarishaji wa mipaka ya kimataifa Jumatano Agosti 27, 2014.
Wasanii wa ngoma ya utamaduni kutoka Burundi wakiburudisha kwenye sherehe za uzinduzi wa programu ya uimarishaji wa mipaka ya kimataifa Jumatano Agosti 27, 2014.
Rais Pierre Nkurunzinza wa Burundi akisalimiana na baadhi ya Watanzania walikuwepo eneo la mpaka kati ya Tanzania na Burundi la Mugikomero wilayani Ngara mkoani Kagera kwa upande wa Tanzania na eneo la Nteritare kwa upande wa Burundi kuhudhuria sherehe za uzinduzi wa programu ya uimarishaji wa mipaka ya kimataifa Jumatano Agosti 27, 2014.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Rais Pierre Nkurunzinza wa Burundi wakipokea nyimbo za Taifa za nchi zao eneo la mpaka kati ya Tanzania na Burundi la Mugikomero wilayani Ngara mkoani Kagera kwa upande wa Tanzania na eneo la Nteritare kwa upande wa Burundi wakati wa sherehe za uzinduzi wa programu ya uimarishaji wa mipaka ya kimataifa Jumatano Agosti 27, 2014.
Sehemu ya umati wa wananchi wa Tanzania na Burundi kwenye sherehe za uzinduzi wa programu ya uimarishaji wa mipaka ya kimataifa Jumatano Agosti 27, 2014.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akihutubia wananchi wa Tanzania na Burundi katika eneo la mpaka kati ya Tanzania na Burundi la Mugikomero wilayani Ngara mkoani Kagera kwa upande wa Tanzania na eneo la Nteritare kwa upande wa Burundi wakati wa sherehe za uzinduzi wa programu ya uimarishaji wa mipaka ya kimataifa Jumatano Agosti 27, 2014.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa meza kuu pamoja na Waziri wa Ardhi na Maendeleo na Makazi, Profesa Anna Tibaijuka, Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo na Naibu Katibu Mkuu Wizara Uchukuzi Dkt Charles Tizeba eneo la mpaka kati ya Tanzania na Burundi la Mugikomero wilayani Ngara mkoani Kagera kwa upande wa Tanzania na eneo la Nteritare kwa upande wa Burundi wakati wa sherehe za uzinduzi wa programu ya uimarishaji wa mipaka ya kimataifa Jumatano Agosti 27, 2014.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete Rais Pierre Nkurunzinza wa Burundi katika picha ya kumbukumbu na wataalamu wa Tanzania na Burundi eneo la mpaka kati ya Tanzania na Burundi la Mugikomero wilayani Ngara mkoani Kagera kwa upande wa Tanzania na eneo la Nteritare kwa upande wa Burundi kuhudhuria sherehe za uzinduzi wa programu ya uimarishaji wa mipaka ya kimataifa Jumatano Agosti 27, 2014.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Rais Pierre Nkurunzinza wa Burundi wakiangalia moja ya alama katika eneo la mpaka kati ya Tanzania na Burundi la Mugikomero wilayani Ngara mkoani Kagera kwa upande wa Tanzania na eneo la Nteritare kwa upande wa Burundi wakati wa sherehe za uzinduzi wa programu ya uimarishaji wa mipaka ya kimataifa Jumatano Agosti 27, 2014. Kushoto kwa Rais Kikwete ni Waziri wa Ardhi na Maendeleo na Makazi, Profesa Anna Tibaijuka
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Rais Pierre Nkurunzinza wa Burundi wakitembelea eneo la mpaka kati ya Tanzania na Burundi la Mugikomero wilayani Ngara mkoani Kagera kwa upande wa Tanzania na eneo la Nteritare kwa upande wa Burundi wakati wa sherehe za uzinduzi wa programu ya uimarishaji wa mipaka ya kimataifa Jumatano Agosti 27, 2014. Kushoto kwa Rais Kikwete ni Waziri wa Ardhi na Maendeleo na Makazi, Profesa Anna Tibaijuka
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Rais Pierre Nkurunzinza wa Burundi wakiangalia moja ya alama katika eneo la mpaka kati ya Tanzania na Burundi la Mugikomero wilayani Ngara mkoani Kagera kwa upande wa Tanzania na eneo la Nteritare kwa upande wa Burundi wakati wa sherehe za uzinduzi wa programu ya uimarishaji wa mipaka ya kimataifa Jumatano Agosti 27, 2014. Kushoto kwa Rais Kikwete ni Waziri wa Ardhi na Maendeleo na Makazi, Profesa Anna Tibaijuka
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Rais Pierre Nkurunzinza wa Burundi wakipata maelezo na kuangalia vifaa vya upimaji eneo la mpaka kati ya Tanzania na Burundi la Mugikomero wilayani Ngara mkoani Kagera kwa upande wa Tanzania na eneo la Nteritare kwa upande wa Burundi wakati wa sherehe za uzinduzi wa programu ya uimarishaji wa mipaka ya kimataifa Jumatano Agosti 27, 2014. Kushoto kwa Rais Kikwete ni Waziri wa Ardhi na Maendeleo na Makazi, Profesa Anna Tibaijuka.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Rais Pierre Nkurunzinza wa Burundi wakizindua kwa pamoja eneo la mpaka kati ya Tanzania na Burundi la Mugikomero wilayani Ngara mkoani Kagera kwa upande wa Tanzania na eneo la Nteritare kwa upande wa Burundi wakati wa sherehe za uzinduzi wa programu ya uimarishaji wa mipaka ya kimataifa Jumatano Agosti 27, 2014.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Rais Pierre Nkurunzinza wa Burundi wakichanganjya udongo na kujenga kwa pamoja alama katika eneo la mpaka kati ya Tanzania na Burundi la Mugikomero wilayani Ngara mkoani Kagera kwa upande wa Tanzania na eneo la Nteritare kwa upande wa Burundi wakati wa sherehe za uzinduzi wa programu ya uimarishaji wa mipaka ya kimataifa Jumatano Agosti 27, 2014.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Rais Pierre Nkurunzinza wa Burundi na wananchi wa nchi zao wakisimama wakati nyimbo za Taifa za Burundi na Tanzania zikipigwa katika eneo la mpaka kati ya Tanzania na Burundi la Mugikomero wilayani Ngara mkoani Kagera kwa upande wa Tanzania na eneo la Nteritare kwa upande wa Burundi wakati wa sherehe za uzinduzi wa programu ya uimarishaji wa mipaka ya kimataifa Jumatano Agosti 27, 2014.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Rais Pierre Nkurunzinza wa Burundi wakijipatia chakula cha mchana katika eneo la mpaka kati ya Tanzania na Burundi la Mugikomero wilayani Ngara mkoani Kagera kwa upande wa Tanzania na eneo la Nteritare kwa upande wa Burundi wakati wa sherehe za uzinduzi wa programu ya uimarishaji wa mipaka ya kimataifa Jumatano Agosti 27, 2014.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Rais Pierre Nkurunzinza wa Burundi wakiagana katika eneo la mpaka kati ya Tanzania na Burundi la Mugikomero wilayani Ngara mkoani Kagera kwa upande wa Tanzania na eneo la Nteritare kwa upande wa Burundi wakati wa sherehe za uzinduzi wa programu ya uimarishaji wa mipaka ya kimataifa Jumatano Agosti 27, 2014.

PICHA NA IKULU
 Kaimu mwenyekiti wa Uukwaa la Katiba Tanzania Hebron Mwakagenda akizungumza na wanandishi wa habari leo Agosti 27, 2014 juu ya mwenendo wa bunge la katiba.

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam.

Wakati mchakato wa katiba Tanzania ukiwa ni kama kitendawili kisicho na majibu sahihi kutokana na mchakato huo kuvurugika na kukosa mwelekeo, nao Jukwaa la Katiba Tanzania (JUKATA) wazidi kumtupia lawama zote za kuvurugika bunge hilo mwenyekiti wa bunge hilo mheshimiwa Samweli Sitta na kudai kuwa ndiye aneyeuvuruga mchakato huo baada ya kugeuza Bunge hilo kama kikao cha Chama cha Mapinduzi (CCM).

Akizungumza na wanahabari muda huu jijini Dar es salaam kaimu mwenyekiti wa Jukwaa la Katiba Tanzania Hebron Mwakagenda amesema kuwa JUKATA wamekuwa wakifuatilia mchakato huu wa bunge ka katiba kwa wiki mbili hizi na kubaini mapungufu makubwa sana ambayo yanatokea jambo ambalo linaonyesha wazi kuwa mwenyeikiti wa bunge hilo hana nia wala dhamira ya kulipatia taifa katiba mpya ya watanzania.

Wanahabari mbalimbali wakiwa wanamsikiliza kiongozi huyo wakati wa mkutano Bw Mwakadenga amesema kuwa swala la mahudhurio ya wabunge wanaoshiriki katika kamati mbalimbali za bunge hilo yamekuwa madogo sana na yasiyo ya kuridhisha ikiwa ni pamoja na wabunge wengi kutokuhudhuria katika kamati hizo pamoja na kusaini kulipwa posho za siku jambo ambalo amesema kuwa ni wizi mpya kwa
watanzania,
 “Kwanza bunge la katiba linaonyesha kuwa wajumbe 441 wamehidhuria lakini uchunguzi wetu unaonyesha kuwa hawa ni wale wote ambao wamewahi kufika na kusaini kwenye kitabu cha mahudhurio wengine wao takribani 100 tuligundua kuwa hawapo bungeni wakiwemo mawaziri wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na serikali ya mapinduzi Zanzibar pamoja na baadhi ya viongozi wa kamati”amesema Mwakagenda.

Ameongeza kuwa mambo mengine ambayo yanalifanya bunge hilo kuvurugika ni pamoja na kukosekana kwa muafaka na maridhiano ya kitaifa, matumizi mabaya fedha ikiwa ni pamoja na Wajumbe kulipwa bila kuhudhuria bungeni, kukosekana kwa theluthi mbili toka Zanzibar ili kupitisha katiba,pamoja na uondoaji wa vifungu muhimu kwenye rasimu mambo ambayo amesema kuwa mwenyekiti Samweli Sitta ameyafumbia macho na kijifanya kama hayaoni huku akiwa anajua wazi kuwa anauzika mchakato huo.

“Huyu mzee hatujamwelewa kabisa, sisi tumekaa tumezungumza naye tukamuuliza atueleze swala la theluthi mbili hawa wajumbe watapatikana wapi hajatupa jibu la kuridhisha na ukimwona ni kama mtu ambaye
ameshachanganyikiwa, anapambana na kila anayekuja mbele yake, iwe mwandishi, mwanaharakati, mbunge, yeye amekaa kujihami tu, sasa hali hii sio nzuri kwa mchakato muhimu kama huu”alisema kiongozi huyo wa JUKATA.
Katika hatua nyingine JUKATA wamemwomba raisi Kikwete kiusimamisha mchakato huu wa katiba hadi kipindi kingine kutokana na kuonekana wazi kuwa hauwezekani na kusema Tanzania imekuwa na michakato mingi ambayo sisi kama taifa hatuwezi kuiendesha kwa wakati mmoja na kupata katiba bora, “Kusema ukweli taifa sasa lina michakati mingi sana mfano mchakato wa vitambulisho vya taifa, uchaguzi wa serikali za mitaa, daftari la kudumu la kupiga kura na michakato mingine mikubwa, hii haitaki usome sana ndo uelewe ni kutumia busara tu kwamba huu mchakato wa katiba hautawezekana tena, sisi tunamwomba mheshimiwa Rais Kikwete awasikilize watanzania na kuusimamisha mchakato huu wa katiba ili tujipange upya kuanza
tena.

Mchakato wa katiba umekuwa ukiendelea jijini Dodoma bila ya mariano na wajumbe waliotoka wa UKAWA huku kukiwa na taarifa kuwa rais amekubali kukutana nao wiki hii kwa ajili ya mazungumzo ya kuunasua mchakato huu.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete (katikati) akiwa na Waziri wa Ujenzi Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli, Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi Mhandisi Mussa Iyombe pamoja na Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu Profesa Juma Kapuya akiweka jiwe la Msingi kuashiria uzinduzi rasmi wa ujenzi wa Barabara ya Magole-Turiani –Mziha sehemu ya Magole-Turiani (48.6km) inayojengwa kwa kiwango cha lami.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na Waziri wa Ujenzi Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli, Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi Mhandisi Mussa Iyombe, mbunge wa Mvomero Amos Makalla, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Joel Bendera pamoja na Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu Profesa Juma Kapuya akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa ujenzi wa barabara ya Magole-Turiani (48.6km).
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara nchini TANROADS Mhandisi Patrick Mfugale akitoa maelezo ya kina kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete kuhusu ujenzi wa Barabara ya Magole-Turiani (48.6km).
Waziri wa Ujenzi Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli wa kwanza kulia akiwa pamoja na Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi Mhandisi Mussa Iyombe kabla ya uzinduzi rasmi wa ujenzi wa barabara ya Magole-Turiani (48.6km) kwa kiwango cha lami.
Waziri wa Ujenzi Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli (katikati) akiwa na Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu Profesa Juma Kapuya wakifurahia jamabo na Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Mheshimiwa Antony Mbasa kabla ya uzinduzi wa Barabara ya Magole-Turiani (48.6km).
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete (kulia) akiwa pamoja na Waziri wa Ujenzi Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli kushoto wakifurahia kikundi cha ngoma za asili mara baada ya Mheshimiwa Rais kuwasili Wilaya ya Mvomero kwa ajili ya kuzindua ujenzi wa Barabara ya Magole-Turiani (48.6km).
Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi Mhandisi Mussa Iyombe wa kwanza (kushoto) akizungumza kabla ya uzinduzi rasmi wa barabara ya Magole Turiani. Wa kwanza kulia kwake ni Mkurugenzi wa Barabara kutoka Wizara ya Ujenzi Mhandisi Ndyamukama pamoja na Mkurugenzi wa Huduma za Ufundi na Umeme Dkt. Wiliam Nshama.