Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Meck Sadick anatangaza rasmi leo Agosti 18, 2015 kuwa mkoa wa Dar es Salaam kuna ugonjwa wa kipindupindu, watu 24 wamelazwa baada ya kubainika kuwa na ugonjwa huo. Watu wawili (mwanamke 1 na mwanaume 1) wameshakufa.
Ugonjwa huo unasambaa kwa kasi katika wilaya ya Kinondoni kwenye kata za Kijitonyama, Kimara, Tandale na nyinginezo na kufanya jumla ya kata 9.
JIHADHARI KULA KULA OVYO MITAANI, WEKA MAZINGIRA YAKO SAFI NA PIA NAWA MIKONO YAKO MARA KWA MARA.



Toa Maoni Yako:
0 comments: