Meneja wa baa ya Safari resort Kimara Bw. Robert Herman akielezea furaha yake baada ya baa yake kutembelewa na promosheni ya Tusker Fanyakweli Kiwanjani huku akifafanua kuwa kiwanja hicho kilichopo Kimara jijini Dar es salaam ni mahali tulivu sana kwa wateja. Baa hiyo iliibuka mshindi wa wiki kwenye kampeni ya Fanyakweli Kiwanjani inayoendeshwa na bia ya Tusker.
 Mshereheshaji wa promosheni ya Tusker Fanyakweli Kiwanjani Gadner G. Habash akielezea utaratibu wa utoaji zawadi kwa wapenzi wa bia ya Tusker waliofika katika baa ya Kisuma wakati wa kuipongeza baa hiyo iliyopo Tandika jijini Dar es salaam. Baa hiyo ilibuka mshindi wa wiki kwenye kampeni ya Fanyakweli Kiwanjani inayoendeshwa na bia ya Tusker lengo likiwa ni kuhamasisha baa mbalimbali za mitaa tunayoishi kufanya kweli pale wanapotoa huduma kwa wateja.
 Mkazi wa Mwembeyanga Bw. Frank Kabisi (katikati) akifurahia zawadi yake ya mfuko na Tisheti alizopewa wakati wa wa hafla ya kuipongeza baa ya Kisuma iliyopo Mwembeyanga Tandika mara baada ya baa hiyo kuibuka mshindi wa wiki kwenye kampeni ya Tusker Fanyakweli Kiwanjani inayoendeshwa na bia ya Tusker toka kampuni ya bia ya Serengeti. (Kushoto) ni Mshereheshaji wa promosheni ya Fanyakweli Kiwanjani na Tusker Gadner Habbash na (kulia) ni balozi wa bia hiyo Bi. Veronica Mbilinyi.
 Msimamizi wa Mauzo wa Kampuni ya bia ya Serengeti kanda ya Ubungo Bw. Victor Mhindi akikabidhi zawadi ya polo shirt kwa Papaa Mazengo mkazi wa Kimara wakati wa promosheni ya Fanyakweli kiwanjani katika baa ya Safari resort. Baa hiyo iliibuka mshindi wa wiki wa shindano hilo baada ya kupigiwa kura na wateja wa baa hiyo. (Kushoto) ni mshereheshaji wa promosheni hiyo Gadner G. Habash.
 Mkazi wa Temeke Bi. Sikudhani Idd akituma salamu kwa marafiki zake kupitia redio Efm iliyokuwa ikisikika moja kwa moja kwenye kiwanja cha Kisuma wakati wa kuipongeza baa hiyo ya Tandika jijini Dar es salaam baada ya baa hiyo kuibuka mshindi wa wiki kwenye kampeni ya Fanyakweli Kiwanjani inayoendeshwa na bia ya Tusker lengo lake likiwa ni kuhamasisha baa mbalimbali za mitaa tunayoishi kufanya kweli pindi wanapotoa huduma kwa wateja. (Kushoto) ni Mshereheshaji wa promosheni ya Fanyakweli Kiwanjani Gadner Habbash na (kulia) ni balozi wa bia hiyo Bi. Veronica Mbilinyi.
Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: