Muonekano wa Daraja jipya la Salenda litaakalopita baharini kuanzia Coco Beachi (Oysterbay) kwenda Hospitali ya Aga Khan  (Maeneo ya Ocean Road/ Baraka Obama Road). Daraja hilo pamoja na barabara zake, litakuwa na urefu wa kilomita 7.2 na uwezo wa kupitisha magari zaidi ya 61,000 kwa siku huku likiwa na njia nne za magari pamoja service road njia za waenda kwa miguu kila upande
Waziri wa Ujenzi Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli kulia akizungumza na Balozi wa Jamhuri ya Korea nchini, Chung Il wapili kushoto kuhusiana na mambo mbalimbali kuhusu sekta ya Ujenzi pamoja na mchakato wa Ujenzi wa Daraja jipya la Salenda litakalopita baharini. Wa kwanza kushoto ni mke wa Balozi huyo.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi Eng. Musa Iyombe kushoto akizungumza na Balozi wa Jamhuri ya Korea Chung Il kulia. Katikati ni Eng. Consolata Ngimbwa, Mwenyekiti wa Bodi ya Makandarasi nchini (CRB).
Waziri wa Ujenzi Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli kushoto akimkabidhi zawadi Balozi wa Jamhuri ya Korea, Chung Il mara baada ya hafla ya chakula cha jioni iliyoandaliwa na Balozi huyo kwa Mheshimiwa Waziri wa Ujenzi.
Mtendaji Mkuu wa TANROADS Eng. Patrick Mfugale akikaribishwa na Mke wa Balozi wa Jamhuri ya Korea. Kulia ni Balozi huyo Chung Il.
Mkurugenzi wa Miradi wa TANROADS Eng. Victor Seff akisalimiana na Mke wa Balozi.
Waziri wa Ujenzi Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akisaini kitabu cha wageni nyumbani kwa Balozi wa Jamhuri ya Korea, Masaki jijini Dar es Salaam.
Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: