Marehemu Mfalme Abdullah bin Abdulaziz enzi za uhai wake.
Mfalme Abdullah bin Abdulaziz akiwa na Rais wa Marekani, Barack Obama.
---
 MFALME wa Saudi Arabuia, Abdullah bin Abdulaziz  amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 90.

Mfalme Abdullah aklikuwa amelazwa hospitalini kwa matibabu ya maradhi yalikuwa yakimkabili tangu m, wezi Desemba mwaka jana.

Kufuatia kifo chake Mdogo wake aitwaye, Salman, 79, amemrithi katika ufalme huo.

Kifo chake kilithibishwa jana katika matangazo katika televisheni ya taifa ambapo ilikuwa ikitolewa mistari  Quran ambayo hutolewa tu endapo kuna kifo cha mtu mzito katika familia ya kifalme.

Mazishi ya Mfalm,e Abdullah yanataraji kufanyika leo kwa kufuata tamaduni za kiislamu ambapo mtu hutakiwa kuzikwa ndani ya saa 24 tangu kifo chake.

Viongozi mbalimbali Duniani akiwemo Rais Barack Obama ametuma salamu za rambi rambi.
Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: