1. Hupiga simu mara kwa mara kumuulizia mpenzi wake anaendeleaje.

2. Hujihisi vibaya pale anaposahau siku ya kuzaliwa (birthday) au siku mliyoanza mahusiano (anniversary) na huomba msamaha.

3. Hushukiza na zawadi mbalimbali hata kama sio muda maalumu.

4. Mara kwa mara hukuambia "NAKUPENDA">>>"I Love You".

5. Anajua kufanya mapenzi na wewe.

6. Anajua jijnsi ya kujali, kukumbatia, kuchumu na kutimiza mahitaji ya kimahaba kwa mpenzi wake.

7. Huhisi kuumia pale mpenzi wake anapopitia hali ngumu.

8. Hupenda kuona mpenzi wake ana furaha na hutamani kufurahi pamoja.

9. Siku zote hutafuta muda mzuri kutumia pamoja na mpenzi wake.

10. Kamwe hawezi kumpiga au kumuumiza kisaikolojia mpenzi wake.

11. Huoa bila kusubiria sanaaaa...

12. Husamehe na kusahau pale anapoumizwa hisia zake.

13. Hatotumia siri au udhaifu wako kukufanyia mabaya.

14. Hatotangaza kama mpenzi wake ana madhaifu fulani.

15. Ni mvumilivu na tayari kufanyia usulihisho kwenye matatizo ya uhusiano wake.

16. Anajua kwamba ni muhimu kwa mpenzi wake kutumia muda wake akiwa na marafiki zake, ndugu na familia yake.

17. Kamwe hawezi kutoka nje ya uhusiano wenu ( will not cheat on you).

18. Hawezi kuwachokoza marafiki zako wakike mpaka point ambayo itakuwa inakuboa au kukupa mashaka.

19. Hawezi kwenda nje ili mfanye mpenzi wake apate wivu.

20. Humheshimu mpenzi wake pale awapo na marafiki na familia yake.

21. Humsaidia mpenzi wake na kazi mbali mbali (mfano za nyunbani au masomo).

22. Hufurahia kampani ya marafiki na ndugu wa mpenzi wake.

23. Husaidia kufikia malengo na kutimiza ndoto za mpenzi wake.

24. Kamwe hakatishi tamaa mpenzi wake pale wanapokuwa wanaongea.

25. Hujali sana kuhusu mawazo, hisia na ushauri wa mpenzi wake.

26. Mara nyingi huwepo pale mpenzi wake anapohitaji msaada.

27. HUJUA KWAMBA NJIA YAKE SIO NJIA PEKEE...

Imeletwa kwenu na Fred Kihwele.
Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

1 comments: