Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba kwa ushirikiano na Dhamana ya Uwekezaji Tanzania (UTT) pamoja na Benki ya Posta Tanzania (TPB), inafurahi kutoa orodha ya awamu ya tatu kwa waliopata viwanja. Orodha hii ni kwa maeneo ya Ihungo, Rwome, Rwazi, Mugeza na Ijuganyondo.

Wote waliopata viwanja kwenye maeneo tajwa wanaombwa kuzingatia mambo muhimu yafuatayo:

  1. Kukamilisha malipo ya kiwanja alichopata kupitia matawi ya Benki ya Posta:

Waliopata viwanja watembelee tawi lolote jirani la Benki ya Posta Tanzania kukamilisha malipo ya kiwanja (yaani Gharama halisi ya kiwanja kutoa gharama ya dhamana iliyowekwa wakati wa kuomba kiwanja).
NB: Ikumbukwe bei ya kiwanja inauzwa kwa mita ya mraba kama ifuatavyo:

ENEO
MATUMIZI
BEI KWA MITA YA MRABA,Tshs
Rwome, Rwazi, Mugeza na Ijuganyondo
Makazi na maeneo ya kuabudia
3,000
Biashara na Taasisi
3,300
Ihungo
Makazi na maeneo ya kuabudia
3,400
 
Biashara na Taasisi
3,600
        
Kwa mfano, malipo ya kiwanja cha makazi cha Rwome, Rwazi, Mugeza na Ijuganyondo chenye ukubwa wa 500m2 gharama inakokotolewa kama ifuatavyo:-
(500m2 x 3,000) – Dhamana. Kwa hiyo gharama yake itakuwa ni
1,500,000-200,000 = Tshs.1, 300,000

  1. Muda wa kukamilisha malipo:
Kila aliyepewa kiwanja atapaswa kufanya malipo haya katika benki ya Posta kuanzia tarehe 01 Novemba, 2012 hadi 30 Novemba, 2012.
NB: Taarifa ya malipo (kwa atakayehitaji ufafanuzi zaidi) inapatikana katika matawi ya Benki ya Posta au Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba kupitia simu 0689469965
  1. Stakabadhi ya malipo kutolewa na Benki ya Posta:
Baada ya kukamilisha malipo, tawi husika la Benki ya Posta litawajibika kutoa stakabadhi ya malipo yenye mhuri wa Benki ya Posta.
  1. Kuoneshwa viwanja kwa waliopata viwanja:
Kwa wale waliofanikiwa kupata viwanja na kama watapenda kuoneshwa viwanja vyao, watapaswa kufika Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba, Idara ya Mipango Miji kwa ajili ya kuoneshwa maeneo yao baada ya kukamilisha malipo.
Ratiba ya kuoneshwa inapatikana Idara ya Mipango Miji na Ardhi Manispaa ya Bukoba.
  1. Orodha ya watakaopata/watakaogawiwa viwanja awamu ya nne:
Zoezi la uchambuzi wa maombi mengine yaliyosalia kwa maeneo yote au pokelewa hadi tarehe 31 Octoba,2012 linaendelea. Orodha hii itatolewa kabla ya tarehe 30 Novemba 2012.
  1. Waliopata viwanja kwenye maeneo ya chaguo la pili:
Kutokana na kuwa na waombaji wengi wa viwanja kwenye baadhi ya maeneo, baadhi ya waombaji imelazimika kuwapeleka katika maeneo ya chaguo lao la pili au la tatu   kama walivyobainisha katika fomu za maombi ya viwanja.
  1. Maandalizi ya Hati miliki ya kiwanja:  
Hati miliki ya kiwanja itaandaliwa kwa wale ambao wamekamilisha malipo ya kiwanja. Mara baada ya kukamilisha malipo ya kiwanja, kila aliyepata kiwanja atapaswa kujaza tena majina yake kikamilifu, anwani na saini yake vitakavyotumika kuandaa hati miliki ya kiwanja. Taarifa hizi zitajazwa kwenye fomu inayopatikana benki ya Posta ambapo malipo yamefanyika.

Kama picha itatofautiana na ile iliyopo kwenye fomu ya maombi ya kiwanja, aliyepata kiwanja atapaswa kufika ofisi za Manispaa ya Bukoba kutoa uthibitisho wa mabadiliko hayo.

  1. Orodha ya waliopata viwanja katika maeneo tajwa hapo juu ni kama ifuatavyo:

Namba ya fomu
Jina la mwombaji
Eneo alilopata kiwanja
Kitalu (Block No)
Namba ya kiwanja
Ukubwa wa eneo
           
Orodha imetayarishwa  kwa kufuata alphabeti za majina.

Tangazo hili linapatikana kwenye tovuti ya UTT Tanzania na ya Mkoa wa Kagera pamoja na mtandao wa jamii wa Bukobawadau.

Muhimu:
  1. Wale wote waliopata viwanja katika awamu ya kwanza na ya pili yaani kwa maeneo ya Kagondo, Nyanga, Kyasha, Buhembe, Nshambya na Makongo muda wa kufanya malipo umeongezwa hadi tarehe 30 Novemba 2012 kutokana na maombi mengi ya waliopata viwanja.

  1. Wale watakaoshindwa kulipa kwa muda huo ulioongezwa Halmashauri itakuwa na hiari ya kugawa viwanja kwa watu wengine bila ya taarifa nyingine.

 Karibu tuijenge upya Bukoba.


Hamisi Kaputa
MKURUGENZI  WA MANISPAA
BUKOBA
Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: