IMG 9338 Naibu Waziri wa Uchukuzi, Dk. Charles Tizeba akisalimiana na Viongozi wa Mamlaka ya Viwanja Vya Ndege Tanzania (TAA), wakati alipofanya ziara katika Kiwanja cha Mwl. Julius Nyerere jijini Dar es Salaam Leo, kujionea shughuli Mbalimbali zinazofanywa na Mamlaka hiyo. Nyuma ya Waziri wa Uchukuzi ni Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka hiyo, Mhandisi. Suleiman Suleiman.
Naibu Waziri wa Uchukuzi,Dk. Charles Tizeba(mwenye suti nyeusi) akiangalia eneo la Kipunguni B ambalo lilifanyiwa tathmini kwa ajili ya kuongeza eneo la Kiwanja cha Ndege cha Mwl. Julius Nyerere jijini Dar es Salaam.
 Naibu Waziri wa Uchukuzi,Dk. Charles Tizeba akipata maelezo ya namna kituo cha hali ya Hewa kinavyofanya kazi katika utoaji wa Taarifa mbalimbali za hali ya Hewa katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwl. Julius Nyerere jijini Dar es Salaam kutoka kwa Bi. Pamela Gabriel kutoka Mamlaka ya Hali ya hewa Tanzania (TMA).Naibu Waziri wa Uchukuzi alifanya Ziara hiyo kujionea shughuli mbalimbali zinazofanywa katika Uwanja huo leo.
Naibu Waziri wa Uchukuzi,Dk. Charles Tizeba akipata malezo kutoka kwa Afisa kutoka Mamlaka ya Usafiri wa Anga(TCAA), Bw. Elieza Mwalutende, wakati Naibu Waziri huyo alipotemmbelea Uwanja Wa Ndege wa Kimataifa wa Mwl . Julius Nyerere jijini Dar es Salaam kujionea shughuli mbalimbali zinazofanywa katika kiwanja hicho.
Naibu Waziri wa Uchukuzi, Dk. Charles Tizeba (aliyeweka mikono miwili mfukoni) akipata maelezo ya namna kikosi cha zima Moto katika Uwanja wa Ndege wa Mwl Julius Nyerere kinavyofanya kazi,Wakati wa Ziara yake hii leo Katika uwanja Huo.
Waziri wa Uchukuzi,Dk. Charles Tizeba (aliyeweka mkono mfukoni) akipata maelezo ya namna Genereta za Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzani(TAA) zinavyofanywa kazi endapo umeme utakatika kutoka kwa Bi. Rehema Ahmed (mwenye Hijabu), wakati wa Ziara yake katika uwanja huo leo.
Hayo ni Majenereta yanayotumika endapo Umeme wa TANESCO unapokatika katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijjini Dar es Salaam.
Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: