Shamba la Malonje linalomilikiwa na Kanisa la Efatha limepata hasara
kubwa baada ya wananchi wa kijiji cha Sikaungu wilayani Sumbawanga
vijijini mkoani Rukwa, kujichukulia sheria mkononi na kuvamia moja ya
kambi ya Shamba hilo iitwayo Sikaungu na kuyateketeza kabisa matrekta
mawili makubwa aina ya New Holland na kubomoa baadhi ya nyumba kwenye
kambi hiyo.
Mchungaji Kiongozi Michael Meela wa Kanisa la Efatha mkoani Rukwa akiongelea kuhusu suala hilo alisema hasara iliyopatikana ni zaidi ya shilingi milioni 228 na kwamba tukio hilo lilitokea mara tu baada ya Mbunge wa Jimbo la KwelaMh. Ignas Malocha kuhutubia mkutano wa hadahara kijijini hapo na kuwahamasisha wananchi watumie nguvu ya umma kuyakomboa mashamba yao yaliyochukuliwa na mwekezaji huyo.
Mchungaji Kiongozi Michael Meela wa Kanisa la Efatha mkoani Rukwa akiongelea kuhusu suala hilo alisema hasara iliyopatikana ni zaidi ya shilingi milioni 228 na kwamba tukio hilo lilitokea mara tu baada ya Mbunge wa Jimbo la KwelaMh. Ignas Malocha kuhutubia mkutano wa hadahara kijijini hapo na kuwahamasisha wananchi watumie nguvu ya umma kuyakomboa mashamba yao yaliyochukuliwa na mwekezaji huyo.

Kamanda
wa polisi wa mkoa wa Rukwa Bw. Jacob Mwaruanda akithibitisha kuhusu
sakata hilo alisema tayari wanawashikilia watu 11 kwa tuhuma za kufanya
uharibifu huo mkubwa na kwamba wanatarajiwa kufikishwa wakati wowote
mahakamani.
![]() |
| Baadhi ya matrekta yaliyoteketezwa kama yanavyoonekana |




Toa Maoni Yako:
0 comments: