Kampuni ya simu za mkononi ya Tigo imewazawadia washindi ishirini na nne, kila mmoja shilingi milioni nne, (Tsh. 4,000,000/-) kama washindi wa kwanza wa kila siku ambao wamepatikana katika promosheni inayoendelea ya “Zamu yako Kushinda.”

Halikadhalika washindi wengine arobaini na nane wamezawadiwa kompyuta aina ya laptop za Samsung. Washindi wamepatikana katika kipindi cha siku 24, na jumla ya fedha zilizotumika kulipa washindi  mpaka leo ni Shilingi za Kitanzania milioni 204.
“Tumeridhishwa na namna ambavyo promosheni inaendelea,” alisema Alice Maro, Meneja Mahusiano wa Tigo. “Bado tunazawadi nyingi za kugawa, kwa hiyo tunapenda kuendelea kuwasihi wateja wetu kushiriki,” alisema.

Baadhi ya washindi wa Tsh. 4,000,000/- ni Juliana Deus (Tabata); Esther Elia (Mbezi Beach); Andrew Mwemezi (Mbeya); Petronila Mtatiro (Ukonga) na Julius Yohana Mlacha (Ubungo). 

Baadhi ya washindi wa laptop ni Dini Kaikai (Ilala); Benjamin Jumbe (Dodoma); Mwanate Abdallah (Mbagala); Hezron Chacha Kehongo (Mbezi Beach) na Omar Msuya (Buguruni); George Kessy (Ngara,Kagera).
Washindi wengine wametoka sehemu mbalimbali nchini kama Bukoba, Mwanza, Morogoro, Dodoma, Mtwara, Lindi, Tanga, Moshi, Arusha, Rukwa, Singida and Pwani.

Ili kushiriki mtumiaji wa Tigo anatakiwa kutuma neno “TIGO” kwenda 15571. Gharama kwa kila ujumbe ni Tsh 450. Washiriki wanatakiwa kujikusanyia pointi nyingi ili kujiwekea mazingira mazuri ya kujishindia zawadi. Washiriki pia watazawadiwa zawadi za kutuma ujumbe wa bure kutoka Tigo kwenda mitandao yote Tanzania.

Watumiaji wa mtandao wa Tigo wenye umri chini ya miaka 18, hawaruhusiwi kushiriki. Promosheni hii ni kwa ajili watumiaji wa Tigo watanzania.
Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: