Pichani ni Said Tamimu Ally

Ndugu zangu

Natoa shukrani zangu za dhati na kwa niaba ya familia ya ndugu Said Tamimu Ally. Nashukuru sana kwa wote waliotoa michango yao ya mali na hali kwa ajili  ya kumsaidia ndugu yetu Tamimu. Shukrani pekee ziwaendee ndugu walioko UK, Norway, Muscat, Dar es salaam, Tabora, Arusha na sehemu nyinge nyingi  kwa msaada wao wa hali na mali ikiwemo ushauri na kutoa pole.

Pili ningependa kuwajulisha kuwa kaka Tamimu siyo mtoto nadhani nilipotuma kwenye blog nilisahau kutaja umri. Huyo ni mtu mzima  mwenye mtoto mmoja wa darasa la saba. Mimi siyo mzazi ila nilimfahamu wakati anapata matibabu hospitali ya KCMC Moshi. Baada ya kumuona anatatizo  niliendelea kunfuatilia mpaka alipo pata referal kwenda Ocean Road Hospital. Kwa sasa hali yake inaendelea kuzorota kwani ameniambia alikwisha maliza kupata mionzi 20 ambayo ameandikiwa pale Ocean Road Hospital, anakwenda na kurudi siku ya clinic.

Nashukuru kwa mawazo ya wengi nimeweza kufungua account benki ya NMB Magomeni ambayo msimamizi ni mdogo wake aitwae Fatuma Tamimu. Ametoa idhini account ifunguliwe kwa jina la mdogo wake wa kike kwani mtoto wake ana umri wa chini ya miaka 18. Kwa wale wote waliotumia M-Pesa,Tigo pesa na Western Union nimekabidhi pesa kwa ndugu Tamimu. Kwa niaba yake natoa shukrani za dhati, asanteni sana. Lakini kwa vile tumefungua accout basi watakaoguswa watumie account number hii
20510000732
NMB Magomeni Branch
Fatuma Tamimu

Kama nilivyosema hali ya afya yake siyo nzuri na namba yake ya simu ni hii 0657-584336 anaweza kuzugumza unaweza kumpigia na kuongea naye. Mwenyezi Mungu awazidishie wote
Asante sana
Anna Sangai.
Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: