
Waziri Mkuu wa mstaafu wa Kenya Raila Odinga akiwasili kwenye viwanja vya Shule ya Sekondari Chato Mkoani Geita kwa ajili ya kwenda kumsalimia Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimkaribisha Waziri Mkuu mstaafu wa Kenya Raila Odinga nyumbani kwake Chato mkoani Geita mara baada ya Kuwasili.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akikumbatiana na Waziri Mkuu wa mstaafu wa Kenya Raila Odinga mara baada ya kuwasili nyumbani kwake Chato Mkoani Geita.

Waziri Mkuu wa zamani wa Kenya Raila Odinga akisalimiana na Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli mara baada ya kuwasili Chato.

Waziri Mkuu wa mstaafu wa Kenya Raila Odinga akiwa na Rais John Magufuli, Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli pamoja na Mke wa Raila Odinga Bi. Ida Odinga wakisali kwenye makaburi ya familia ya Mhe. Rais Chato Mkoani Geita.

Waziri Mkuu wa zamani wa Kenya Raila Odinga akisalimiana na mama mzazi wa Rais Dkt. John Pombe Magufuli, Bi Suzana Joseph Magufuli mara baada ya kuwasili Chato Mkoani Geita.
Waziri
Mkuu Mstaafu wa Jamhuri ya Kenya Mheshimiwa Raila Amoro Odinga
amemtembelea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe
Magufuli aliyopo mapumzikoni katika Kijiji cha Kilimani, Wilaya ya Chato
Mkoani Geita.
Mheshimiwa
Odinga ambaye ameongozana na mkewe Mama Ida Odinga na Binti yake Winnie
Raila Odinga, wametua kwa Helkopta katika uwanja wa Shule ya sekondari
ya Chato leo tarehe 02 April, 2016 majira ya saa 11 jioni na baadaye
kuelekea nyumbani kwa Rais Magufuli ambako wamepokelewa na wenyeji wao
Rais Magufuli mwenyewe na Mkewe Mama Janeth Magufuli.
Waziri
Mkuu Mstaafu wa Jamhuri ya Kenya Mheshimiwa Raila Amoro Odinga
amemtembelea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe
Magufuli aliyopo mapumzikoni katika Kijiji cha Kilimani, Wilaya ya Chato
Mkoani Geita.
Mheshimiwa
Odinga ambaye ameongozana na mkewe Mama Ida Odinga na Binti yake Winnie
Raila Odinga, wametua kwa Helkopta katika uwanja wa Shule ya sekondari
ya Chato leo tarehe 02 April, 2016 majira ya saa 11 jioni na baadaye
kuelekea nyumbani kwa Rais Magufuli ambako wamepokelewa na wenyeji wao
Rais Magufuli mwenyewe na Mkewe Mama Janeth Magufuli.
Akizungumza
mara baada ya kuwasili Chato, Mheshimiwa Raila Odinga amesema yeye na
familia yake wapo likizo na wamekuja kumtembelea rafiki wa familia yao,
kwa lengo la kumsalimia.
"Nimekuja
kupumzika na nimekuja na Mama na Mtoto wangu wa kike, na vilevile kuja
kutoa pongezi kwa ndugu yangu kwani tangu achaguliwe sijakuja hapa
Chato, na nilisema siendi Dar es salaam nitakuja hapahapa Chato" Alisema
Mheshimiwa Odinga.
Pamoja
na kukutana na Rais Magufuli na Mkewe Mama Janeth Magufuli, Waziri Mkuu
Mstaafu wa Kenya Mheshimiwa Raila Odinga pia amemsalimu Mama wa Rais
Bibi Suzana Joseph Magufuli na pia amezulu Makaburi walimozikwa
wanafamilia wa Rais, akiwemo Baba Mzazi Mzee Joseph Magufuli.


Toa Maoni Yako:
0 comments: