Katika hali ya kushangaza mtu mmoja mwenye asili ya Kuburushi ambaye jina lake halikuweza kupatikana leo amekamatwa na marundo ya hela kwenye begi ikiwa amefika nazo kwa ajili ya kuzigawa kwa wajumbe wa NEC ili wasusie kikao cha leo hadi pale jina la Mhe. Edward Lowassa litakaporudishwa na kama ikishindikana achaguliwe Mhe. Magufuli.
Kwa mujibu wa uchunguzi uliofanywa na makachero wenu waliopo maeneo mbali mbali ya mji wa Dodoma zinasema kuwa watu hao walikamatwa katika hoteli ya St. Gasper iliyopo nje kidogo ya mji wa Dodoma.
Mpaka sasa hali si shwari kwa mji wa Dodoma maana vijana wengi wamezagaa kila kona huku ulinzi ukiwa umeimalishwa.

Mhindi huyo alishukia kwenye hoteli ya St. Gasper ambayo wapambe wengi wa Lowassa wakiwamo mzee Kingunge ambaye wamepiga kambi.
Huyo Mburushi ni mtumishi wa Caspian ya Rostam Aziz. Wengine walioonekana pichani wamo Fadhili Ngajiro; Ole Porokwa; Omar Ng'wanang'wala.




Toa Maoni Yako:
0 comments: