Mifereji ya maji taka ni finyu nayo ikishinda bila kufanyiwa usafi ikiwa ni pamoja na uzibuaji hali huwa tete.

Adha waipatayo wafanyabiashara waliopangisha kwenye maduka ya majengo yaliyopo pembezoni kwa kituo cha daladala za Mwaloni zamani karibu na soko kuu. Mitaro imejaa, barabara zimejaa maji, Si biashara tena bali sasa ni kila mmoja kuokoa mali zake.

Ili kuepuka kadhia hii ambayo kama mvua ingenyesha nyakati za usiku ingekuwa hasara kubwa kwa mali zilizowekwa sakafuni, basi ni jukumu sasa la kila mfanyabiashara kuhakikisha takataka za maboski, mifuko, vitambaa na bidhaa nyingine za kutupa, kuwa zinahifadhiwa kwenye mapipa maalum ya taka na si kuyaelekeza kwenye mifereji ya maji taka.

Picha zote na Gsego Blog.

Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: