Washiriki wa mkutano wa 7 wa Mapitio ya Utendaji wa sekta ya Uchukuzi, wakijitambulisha kabla ya mkutano huo wa siku mbili kuanza katika ukumbi wa mikutano wa Jengo la Jubilee. Mkutano huo wa 7 unawakutanisha wadau mbalimbali wa sekta ya Uchukuzi kujadili changamoto mbalimbali zinazoikabili sekta na kuzitafutia ufumbuzi.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, Dkt. Shaaban Mwinjaka akitoa hotuba wakati wa ufunguzi wa Mkutano 7 wa mapitio ya utendaji wa Sekta ya Uchukuzi(JTSR 2013), unaofanyika katika ukumbi wa mikutano Jengo la Golden Jubilee tarehe 28-29 Oktoba 2013. Mkutano huo wa 7 unawakutanisha wadau mbambali wa sekta ya uchukuzi kujadili changamoto mbalimbali zinazoikabili sekta ya uchukuzi na kuzitafutia ufumbuzi ili kuboresha Uchukuzi nchini Tanzania.
 Waziri wa Uchukuzi, Dkt. Harrison Mwakyembe akitoa hotuba yake wakati wa ufunguzi wa mkutano wa 7 wa mapitio ya utendaji wa sekta ya Uchukuzi leo asubuhi katika ukumbi wa mikutano uliopo kwenye Jengo la Golden Jubilee(PSPF BUILIDNG). Mkutano huo wa siku mbili unakutanisha wadau wa taasisi mbalimbali za sekta ya uchukuzi kujadili njia mbalimbali za kuboresha sekta ya Uchukuzi.
  Waziri wa Uchukuzi, Dkt. Harrison Mwakyembe (wa tatu kutoka kushoto waliokaa), akiwa katika picha ya pamoja na Mabalozi, wahisani wa Miradi ya Maendeleo na wajumbe mbalimbali waliohudhuria mkutano wa 7 wa mapitio ya utendaji wa sekta ya Uchukuzi, Unaofanyika tarehe 28-29 Oktoba katika ukumbi wa mikutano wa Jengo la Golden Jubilee. Wa kwanza kushoto waliokaa ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, Mrs. Monica Mwamunyange, kulia kwa Waziri Mwakyembe ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, Dkt. Shaaban Mwinjaka.

(Kitengo cha Mawasiliano Serikalini-Uchukuzi)
Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: