Mahakama ya Hakimu Mkazi ya Kisutu, Dar es Salaam imemzuia msanii kutoka Nigeria, Adedeji Adelek maarufu kama ‘Davido’ kuperform katika tamasha la Fiesta linaloandaliwa na Clouds Fm na Prime Promotion, October 18,2014.

Amri hiyo imetolewa jana (October 17) na hakimu mkazi wa mahakama ya kisutu , mheshimiwa D. Kisoka kufuatia maombi ya dharura yaliyowasilishwa mahakamani hapo na Times Fm Radio na Times Fm Promotion.

Times Fm Radio na Times Fm Promotion walipeleka maombi ya dharura mahakamani hapo wakiitaka mahakama kumzuia msanii huyo kuperform katika tamasha hilo kwa kuwa licha ya BASATA (Baraza La Sanaa Tanzania) kukataa kutoa kibali cha msanii huyo kwa maelezo kuwa tayari alikuwa ameshachukuliwa kibali cha kuperform nchini November 1 kwenye tamasha lililoandaliwa na Times Fm Radio,  Clouds Fm na Prime Times Promotion waliendelea na taratibu zote bila kujali zuio hilo la BASATA.

Times Fm Radio na Times Fm Promotion waliiomba mahakama kuidhinisha madai yao dhidi ya Clouds Fm, Prime Promotion na mkurugenzi wa kampuni inayomsimamia Davido, HKN Music.
Madai hayo ni pamoja na kulipwa fidia ya gharama na usumbufu waliosababishiwa na walalamikiwa kadiri Mahakama itakavyoona inafaa.

Mahakama imetoa amri kuwa msanii huyo amezuiwa kufanya onesho hilo October 18,2014 hadi pale ufumbuzi wa kesi hiyo utakapopatikana Mahakamani hapo.

Awali, Davido alisikika katika matangazo ya Times Fm Radio akieleza kuwa atakuja Tanzania November 1 kwa ajili ya kufanya onesho linaloandaliwa na kituo hicho cha radio lililopewa jina la ‘The Climax’.
Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: