Na Devota Mwachang’a
 
Hatimaye Beatrice Shimende Kantimbo (48) pichani amefanikiwa kusafiri kwenda nchini  India kutibiwa mguu katika hospitali ya Apollo, kutokana na michango ya wasamalia wema pamoja na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii.

Akizungumza muda mfupi kabla ya kuondoka katika uwanja wa ndege wa Julius Nyerere (JNIA) jijini Dar es Salaam hivi karibuni, Beatrice, aliyeambatana na Mumewe Emmanuel Kantimbo aliwashukuru sana wale wote walioguswa mara baada ya kupata taarifa zake, na kuamua kumsaidia kwa pesa, ushauri na kwa sala, pia vyombo vya habari.

Beatrice amesumbuliwa na maradhi hayo kwa takribani miaka 12, vipimo vya kitabibu vimegundua kuwa ni ugonjwa wa matende (elephantiasis).
Mwanamke huyu alikuwa ni 'mchakarikaji' kweli,  aliendesha maisha yake kwa biashara kadhaa wa ikiwemo biashara ya duka, grosari na saluni ya ususi wa nywele pia  aliyekuwa akifanya kazi za ushereheshaji (MC) kwenye sherehe akifahamika kama MC Kimbaumbau,

Hapa alisimulia namna alivyoanza kuugua…"Nakumbuka mwaka 1998 nikiwa kwenye biashara zangu pale Ubungo, kuna kitu kilinichoma hapa (anaonyesh pajani) maumivu yake yalikuwa mithiri ya sindano, hata hivyo hayakudumu sana wala hapakuwa na alama yoyote.

"Baada ya dakika chache nikajihisi homa kali. nikaanza kutetemeka mwili mzima, nikaamua kwenda hospitali ya Neema, hospili ya karibu na mahali nilipokuwa nikiishi pale Ubungo. Daktari akanipima, akagundua nilikuwa na malaria.

"Wakati huo mguu haukuonyesha dalili zozote za maumivu wala jeraha. Malaria ilkuwa kali, nikalazwa kwa muda wa wiki mbili pale hospitali. Nikaruhusiwa, nikarudi nyumbani na hapo ndipo nilipoanza kuona mguu unavimba. Kaadri siku zilivyozidi kwenda ndivyo mguu nau unavimba"

Kuanzia mwaka 2010 mguu umezidi kuongezeka kuvimba na maumivu makali yaliyotokana na kidonda kikubwa kilichosababishwa na kuondolewa kwa sehemu ya nyama ya mguu wake wa kuume iliyokuwa imeoza.

Anasema: "Baadhi ya madaktari wa Muhimbili walinishauri nikubali kukatwa mguu. Wanasema ya nyama imeoza na mfupa wa mguu umeharibika. Mimi sikukukubaliana na ushauri wao kwa sababu baada ya kupigwa X-ray 2007 iligunduliwa tatizo kubwa lilikuwa matatizo kwenye mishipa ya kupitisha maji kutokana na nyama kuharibika. Sio mfupa.

"Nilikataa kwa imani kuwa nitapona tu. Nikijiangalia nina uwezo wa kusimama na kutembea isipokuwa tu kinachonipa taabu kwa sasa ni nyama za mguu zimekua sana kiasi kwamba nikitembea zinagusa mguu wa kushoto" alisema.
Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: