Wanamuziki wa Mapacha Watatu, Kalala Junior (aliyebebwa) na Khaleed Chokoraa, wakionyesha uwezo wao jukwaani hapo. 
 Mwimbaji wa kundi la Super Shine Modern Taarab, Ally Mikidadi, akiwajibika. 
 Bosi wa TOP Bandi, mwanamuziki TID, akiwajibika.
 Msanii Zuhura akipagawisha mashabiki.
 Mr Blu akitoa burudani kwa kila mtu.
 Dogo Hamidu a.k.a Nyandu Tozi akiwa na Mr Blue.
 Dogo Faume akiwajibika. 
 Kundi la Wakali Dancers likitesa jukwaani.
 Msanii wa kucheza na kuigiza, Mpella Shaa ‘Kidevu cha Kuku’ akiwa amekaa juu ya chupa jukwaani hapo.
 Watoto wakiserebuka ukumbini.

Umati uliokuwa ukumbini ukifuatilia burudani hizo. 
---
WASANII wa muziki wa kizazi kipya na dansi Bongo, Khaleed Mohamed ‘TID’, Herry Samir ‘Mr Blu’, wakiwa na kundi la Mapacha Watatu ambalo linaongozwa na Khaleed Chuma ‘Chokoraa’, Junior Kalala ‘Kalala Junior’, na Joseph Michael ‘Jose Mara’, na kundi la muziki wa mwambao la Super Shine,  usiku wa kuamkia leo wamefanya kufuru ndani ya ukumbi wa kisasa wa Dar Live uliopo Mbagala jijini Dar es Salaam.  Wanamuziki hao walivunja rekodi ya mashabiki wengi waliowahi kushuhudia makamuzi kama hayo katika kituo hicho cha burudani nchini. 

Shoo hiyo pia ilisindikizwa na makundi mengine kama Wakali Dancers, na wasaniii wengine wa Bongo Fleva wakiwemo Zuhura na  Dogo Mfaume na Hejos Band. 


Picha na Habari: Musa Mateja/GPL
Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: