Pages

Thursday, 23 July 2015

AIRTEL WAKABIDHI JEZI KWA TIMU ZITAKAZOSHIRIKI MICHUANO YA AIRTEL RISING STARS

Mwenyekiti kamati ya soka la vijana katika Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Ayubu Njenza (kushoto) akimkabidhi vifaa vya michezo katibu wa chama cha mpira wa miguu Wilaya ya Kinondoni,Isaac Mazwile kwaajili ya mashindano ya vijana chini ya umri wa miaka 17 ya Airtel Rising Stars, inayoanza tarehe 24 Julai mkoani Mbeya. katikati ni Afisa Uhusiano Airtel,Jane Matinde. Makabidhiano hayo yalifanyika leo jijini Dar-es-Salaam.
Mwenyekiti kamati ya soka la vijana katika Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Ayubu (katikati kushoto), Afisa Uhusiano Airtel, Jane Matinde, katibu wa chama cha mpira wa miguu Wilaya ya Kinondoni,Isaac Mazwile kulia na Afisa Maendeleo wa TFF bwana Jemadari kwa pamoja wakionyesha vifaa vya michezo vitakavyotumika wakati wa michuano ya Airtel Rising Stars. Airtel jana ilikabithi vifaa kwa timu zote zitakazoshiriki michuano ya Airtel Rising Stars kwa mwaka huu.
Mwenyekiti kamati ya soka la vijana katika Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Ayubu Njenza (kushoto) akimkabidhi vifaa vya michezo katibu wa chama cha mpira wa miguu Wilaya ya Ilala Kanuti Daudi kwaajili ya mashindano ya vijana chini ya umri wa miaka 17 ya Airtel Rising Stars katikati ni Afisa Uhusiano Airtel Jane Matinde. Makabidhiano hayo yalifanyika leo jijini Dar-es-Salaam.

No comments:

Post a Comment