_1055413.JPG-3 Research methodology
Aziz Kilonge Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi Bodi ya Wataalam wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB) ambaye alikuwa mgeni rasmi wakati wa kufunga warsha ya mafunzo ya uandishi bora wa tafiti ili kukidhi hitaji la msingi la kuhitimu taaluma ya ununuzi na ugavi iliyoratibiwa na kuendeshwa na Bodi ya Wataalam wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB) kuazia tarehe 21 julai mpaka 25 julai 2014. kwenye ukumbi wa baraza la maaskofu TEC-Kurasini jijini Dar es salaam akiwa katika [icha ya pamoja na wakufunzi, washiriki pamoja na baadhi ya wakuu wa taasisi hiyo .kulia kwake ni Mtendaji Mkuu wa PSPTB Dr. Clemence Tesha, kutoka kushoto ni Dr. E. Tumsifu-mwezeshaji wa washa na Ally Songoro Mkurugenzi wa Mafunzopamoja na washiriki wa warsha hiyo.
_1055431.JPG-1 research methodology
Bodi ya Wataalam wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB), kulia kwake ni Mtendaji Mkuu wa (PSPTB) Dr. Clemence Tesha, kutoka kushoto ni Dr. E. Tumsifu-mwezeshaji wa washa na Ally Songoro Mkurugenzi wa Mafunzopamoja na washiriki wa warsha hiyo pamoja na wanawarsha.
_1015339.JPG-2-research methodology
Picha ya pamoja ya washiriki na baadhi ya viongozi wa Bodi ya Wataalam wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB) kwa maelezo zaidi kuhusu taarifa mbalimbali za bodi wataalamu wa Ununuzi na Ugavi.
Wasanii wa Tanzania wenye mashabiki wengi Afrika Mashariki, Lady Jay Dee na Diamond Platinumz, wameitoa Tanzania Kimasomaso kwa kushinda tuzo moja moja katika tuzo za AFRIMA (African Muzik Magazine Awards 2014), zilizofanyika jana Dallas, Marekani.

Kwa mujibu wa mtandao wa African Music Magazine, Lady Jay Dee alishinda tuzo ya mwimbaji bora wa kike wa Afrika Mashariki na Diamond Platinumz alishinda tuzo ya Msanii bora wa kiume wa Afrika Mashariki.

Hii ni orodha kamili ya washindi wa AFRIMMA 2014

Best DJ Africa 2014- Dj Black (Ghana)

Best African DJ USA 2014 – Dj Josh (Kenya)

Best Video of the Year 2014- Flavour (Nigeria)

Best Male East Africa 2014- Diamond (Tanzania)

Best Male West Africa 2014- Davido (Nigeria)

Best Female East Africa 2014- Lady Jaydee (Tanzania)

Best Female West Africa 2014 – Tiwa Savage (Nigeria)

Best Male Central Africa 2014 – Fally Pupa (Congo)

Best Female Central Africa 2014- Gasha ( Cameroon)

Best Male Southern Africa 2014- Khuli Chana (South Africa)

Best African Group 2014- P-square (Nigeria)

Best Male Diaspora 2014- Fuse ODG (Ghana)

Best Female Diaspora 2014- Les Nubians (Cameroon)

Best Female Southern Africa 2014- Zahara (South Africa)

Best Dancehall Artist 2014 – Timaya (Nigeria)

Best Dance in a Video 2014- Iyanya (Lekwa Ukwu) (Nigeria)

Best Gospel Artiste 2014- Bahati (Kenya)

Best Traditional Artist 2014- Flavour (Nigeria)

Best Newcomer 2014- Stanley Enow (Cameroon)

Best Video Director 2014- Ogopa Dj’s (Kenya)

Music Producer of the year 2014- Dj Oskido (South Africa)

Best Dance Group 2014- Imagineto (Nigeria)

Best Rap Act 2014- Sarkodie (Ghana)

Best Collaboration 2014- Mafikizolo ft Uhuru (Khona) (South
Africa)

Song of the Year 2014- Kcee (Nigeria)

Artist of the Year 2014- Davido (Nigeria)

Leadership in Music Award 2014- 2face Idibia

Legendary Award 2014- Yvonne Chaka Chaka

Transformational Leadership Award 2014- Chief Dr. Godswill
Akpabio
1
Kiongozi wa Mbio za Mwenge kitaifa Bi Rachel Kasanda akikabidhi mashine za kufyatulia matofali kwa Hassan Soud Katibu wa kikundi cha Changamoto kwa niaba ya vikundi vingine vya wilaya ya Ilala ambazo zimetolewa na shirika la Nyumba nchini NHC jana wakati wa mpokezi ya Mwenge wa Uhuru Ilala Boma mara baada ya Meneja wa Shirika hilo wilaya ya Ilala Bw. Jackson Maagi kumkabidhi kiongozi huyo wa mbio za mwenge ikiwa ni juhudi za shirika hilo kusaidia kupunguza uhaba wa ajira kwa vijana ili waweze kujiajiri kwa kuyatua matofali na kuuza.
3
Askari wa Kikosi cha FFU wakiulinda mwenge mara baada ya kuwasili Ilala Boma mahali ambapo ndiyo kituo ulipolala mwenge huo.
4
Meneja wa Shirika la Nyumba la Taifa NHC Bw. Jackson Maagi wa pili kutoka kushoto akiwa pamoja na wafanyakazi wenzake kabla ya kukabidhi mashine hizo jana.
2
Meneja wa Shirika la Nyumba la Taifa NHC Bw. Jackson Maagi akizungumza wakati wa kukabidhi mashine hizo jana.
---
HOTUBA FUPI YA MENEJA WA NHC ILALA KWA KIONGOZI WA MBIO ZA MWENGE KITAIFA

Ndugu kiongozi wa Mbio za Mwenge,

Ninayo furaha kubwa sana kusimama mbele yenu na kuongea nanyi kama mwakilishi kutoka Shirika la Nyumba la Taifa.

Ndugu Kiongozi wa Mbio za Mwenge; Shirika la Nyumba la Taifa lina mpango mkakati wake wa miaka mitano ambao moja ya malengo yake sita makuu ni kuboresha taswira ya Shirika. 

Katika utekelezaji wa lengo hili, Shirika lina sera ya huduma kwa jamii ambayo imejikita katika kusaidia vijana kujiajiri. Ili kuwezesha vijana kujiajiri, Shirika limeamua kuzisaidia Halmashauri za Miji na Wilaya kote nchini mashine za kuwezesha vikundi vya vijana kutengeneza matofali ya kujengea nyumba. Nchi yetu ina Halmashauri 160 na kila Halmashauri itapewa mashine 4 kwa ajili ya kusaidia vikundi vya vijana. Katika mpango huu jumla ya mashine 640 zitatolewa na Shirika na kugharimu shilingi 288,000,000/. 

Aidha, kila Halmashauri itapatiwa shilingi laki tano (500,000/=) kama mtaji kwa vijana kuanzia shughuli yao ya kutengeneza matofali. Kadhalika, Shirika limegharamia shilingi 800,000/= kwa kila Halmashauri kwa ajili ya kuwalipa wakufunzi kutoka VETA wanaotoa maelekezo kwa vijana namna ya kutumia mashine hizo. 

Ndugu Kiongozi wa Mbio za Mwenge, katika kutekeleza mradi huu jumla ya shilingi milioni mia saba (700,000,000/=) zitatumika. Aidha, tunatarajia kuwa ajira zaidi ya 8,000 za moja kwa moja na ajira nyingine zaidi ya 200,000 zisizo za moja kwa moja zitapatikana. 

Katika mpango huu kila Wilaya inatakiwa kuwa na vijana 40 watakaokuwa katika vikundi vya watu 10 kila kimoja. Msaada huu ni mkubwa lakini kutokana na ukubwa wa tatizo la ajira jitihada zaidi kutoka kwa wadau mbalimbali zinatakiwa. Ni matarajio yetu kuwa taasisi nyingine ama mtu mmoja mmoja atashiriki kukwamua vijana hawa. 

Ndugu Kiongozi wa Mbio za Mwenge, kupitia maadhimisho haya, Shirika linatoa mashine nne (4) kwa vikundi 4 vya vijana vilivyoundwa katika wilaya ya Ilala ambapo kila kikundi kina jumla ya vijana10 watakaotumia mashine moja. Hivyo jumla ya vijana 40 katika Wilaya hii watapata ajira kutokana na mashine hizi. 

Ndugu Kiongozi wa Mbio za Mwenge, mwisho Shirika linatoa rai kwa Taasisi za serikali, mashirika ya umma, binafsi na watu mbalimbali, kuunga mkono juhudi za Serikali za kupunguza tatizo la ajira kwa vijana. Ni matumaini yetu kuwa tutawaunga mkono kwa kununua matofali yao ama kusaidia upatikanaji wa mashine nyingine zaidi ili wengine ambao hawajafikiwa na mradi huu wafikiwe na wapate kufaidika. 

Kipekee tunaomba Serikali za Mitaa (kwa maana ya Halmashauri zetu za wilaya, miji, manispaa ama jiji) wawe ni wanunuzi wakuu wa matofali yatakayotengenezwa na vikundi hivi vya vijana ambayo ni ya gharama nafuu ili kusaidia miradi mbalimbali ya ujenzi na kuwaongezea kipato chao. Tunawaomba pia msaidie kusimamia mradi huu ili uweze kuwa endelevu.
SIKU moja baada ya serikali kufunga Hospitali ya Chuo cha Kimataifa cha Matibabu na Teknolojia (IMTU), kwa madai ya kuendeshwa kwa kukiuka taratibu za tiba, hatua hiyo imefikiwa ili kukinusuru chuo hicho na adhabu ya utupaji viungo vya binadamu.

Kwamba uamuzi huo umefikiwa kutuliza hasira za makundi mbalimbali, kikiwamo Chama cha Madaktari Tanzania (MAT), waliolaani utupaji huo.

Wakati hatua hiyo ikionekana kutaka kunusuru kufungwa kwa chuo, viongozi wa serikali ya wanafunzi chuoni hapo wamesema kikifungwa watakuwa wanaonewa kwakuwa wanaostahili adhabu ni utawala.

Chanzo hicho kimesema kama chuo hicho kingefungwa, ingeathiri wanafunzi wengi ambao wengine wanasubiri kufanya mitihani yao ya mwisho kumaliza elimu yao ya tiba.

Kitendo cha Manispaa ya Kinondoni kufanya ukaguzi huku timu za uchunguzi wa suala hilo zikiwa kazini, kinalenga kutoa ahueni kwa chuo kuendelea na shughuli zake.

Itakumbukwa kuwa serikali iliunda tume ya watu 15 kuchunguza jambo hilo, huku nalo Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam likiteua timu ya kufuatilia watuhumiwa waliohusika na utupaji viungo hivyo.

Imebainika kuwa ufungaji hospitali hiyo unaonekana uliratibiwa mapema kwakuwa wakati timu ya wakaguzi hao ikifika hospitalini hapo, hakukuwa na mgonjwa aliyelazwa tofauti na ilivyo kawaida.

Baadhi ya wafanyakazi walidokeza kuwa adhabu ya kufungwa kwa hospitali hiyo inaweza kukinusuru chuo kwakuwa ripoti itakayotolewa na tume ya watu 15 iliyoundwa na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, inaweza kutoa pendekezo la aina hiyo.

“Adhabu hii ya kufunga hospitali ni kama kinga ya kuunusuru uongozi wa chuo hicho ambao kimsingi na kisheria ndio wanaostahili kufanya kazi za utafutaji, usafirishaji, utunzaji, uhifadhi na kuzika au kuchoma miili hiyo kwa kufuata miiko ya kazi hiyo inavyotaka,” kilisema chanzo hicho.

Juzi timu ya Menejimenti ya Afya ya Manispaa ya Kinondoni, iliyokuwa imeongozana na Mganga Mkuu wa Manispaa, Dk. Gunini Kamba, wameifunga hospitali hiyo baada ya kubaini kuwepo kwa upungufu sehemu mbalimbali.

Alisema upungufu walioubaini ni kutokuwa na wauguzi, vifaa vya kutosha, sehemu ya kuteketeza taka ngumu, wamekuwa wakichanganya dawa zilizokwisha muda na ambazo zinatumika katika kabati moja.

Dk. Gunini alisema: “Upungufu wa madaktari umesababisha tumkute mfanyakazi mmoja wa msalaba mwekundu akifanya kazi za madaktari.”

Alisema kuwa kama viongozi wa IMTU watataka kuendelea na huduma ya hospitali, wanatakiwa kurekebisha matatizo hayo waliyoambiwa ikiwamo kutuma maombi upya kwa kuanzia manispaa.

Rais wa Serikali ya Wanafunzi wa IMTU, Meekson Mambo, alisema tangu sakata hilo lianze, limesababisha wanafunzi kushindwa kusoma kwa uhuru na muda mwingi kuutumia katika kutafakari hatima yao.

Mambo, alisema wanapinga vikali kauli ya Rais wa Chama cha Madaktari Tanzania (MAT), Dk. Primus Saidia ya kutaka serikali ikifute chuo hicho.

Rais huyo alisema kuwa kiongozi wa MAT, alitoa kauli hiyo bila kutafakari kwa kina mustakabali wa uamuzi anaotaka uchukuliwe, kwani hatua hiyo ni sawa na kutaka kuwahukumu wanafunzi wasiohusika na tukio hilo.

Alifafanua kuwa alitarajia Dk. Saidia, angesikiliza maoni ya wanafunzi juu ya tukio hilo na kuwaona viongozi na mmiliki wa chuo kupata ukweli.

Aliongeza kuwa uamuzi wowote utakaofanywa kukifuta chuo hicho utakuwa na athari kubwa kwa wanafunzi, na hawatakubali hatua hiyo.

“Tumeshawaambia watu wanaofanya uchunguzi kuwa hatutakubali wazo la kufutwa kwa chuo au kufungwa… sisi tuna kosa gani, kina nani walitupa viungo?” alihoji.

Waziri Mkuu wa Serikali hiyo, Edward Mhina, alisema jumuiya yao inalaani kitendo cha utupaji wa miili hiyo kwa kuwa inakiuka maadili na sheria za mafunzo ya udaktari.

“Tanzania ina uhaba wa madaktari, MAT inashinikiza chuo hiki kifutwe, tunaelekea wapi? Tuache vyombo vya dola vifanye kazi yake,” alisema.

Mabaki ya miili ya binadamu yaliyokuwa kwenye mifuko 85 ya plastiki, yalikutwa wiki iliyopita yakiwa yametelekezwa maeneo ya Mto Mpiji, Mbweni nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam na haikujulikana mara moja imetoka wapi, kabla ya polisi kufanya uchunguzi.
MKAZI wa Yombo Kilakala jijini Dar es Salaam, Charles Swai (48), amekutwa chumbani kwake akiwa amefariki dunia.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Temeke, Kamishna Msaidizi Mwandamizi (SACP), Englibert Kiondo, alisema tukio hilo lilitokea majira ya saa 8:00 mchana, ambapo mwili wa marehemu ulikutwa kitandani na haukuwa na jeraha lolote.

Kiondo alisema kifo hicho kiligundulika baada ya Swai kutofungua mlango wa chumba chake tangu alipofunga Julai 23 saa 2 usiku, ndipo majirani walipochungulia dirishani na kumuona akiwa amelala na kutoa taarifa Kituo cha Polisi Chang’ombe.

Alisema askari walifika eneo hilo na kuvunja mlango na kumkuta akiwa amefariki dunia. Chanzo cha kifo hakijafahamika na mwili umehifadhiwa hospitali ya Temeke. Upelelezi unaendelea.

Katika tukio jingine, dereva aliyefahamika kwa jina la Felix Mgoba (25) mkazi wa Wazo, amefariki dunia baada ya gari alilokuwa akiendesha kugongana na Fuso.

Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Kamishna Msaidizi (ACP), Camillius Wambura, alisema lilitokea juzi saa 5:20 asubuhi huko barabara ya Bagamoyo eneo la Boko Msikitini.
Na Mnyetishaji Wetu, Mitandao ya Jamii.

Kauli ya Ommy Dimpoz aliyoitoa siku mbili zilizopita akishauri wadau wajitokeze na kuwekeza zaidi katika kununua vifaa vya kisasa ili wasanii wasipate sababu ya kwenda kushoot video zao nje, imewafanya madirector nao kutoa yao ya moyoni.

Kauli ya Ommy Dimpoz imetokana na maswali ambayo watu wengi wamekuwa wakihoji kwanini wasanii wengi sasa hivi wanaamua kwenda kushoot video zao nje na kwa gharama kubwa ili hali inaaminika hapa nyumbani bado kuna maeneo mengi na mazuri ya kufanyia video ambayo hayajatumika.

Baada ya Nisher kuzungumza na kuwatupia lawama wasanii kuwa wanawadharau madirector wa Tanzania, Adam Juma wa Visual Lab na yeye ametoa ya moyoni kuhusu kauli hiyo ya Dimpoz, kupitia Instagram ameandika:

“Hahahahahahha vifaaa tutanunua inshallah, ila sasa nasisi tutaanza kutangaza bei mnazotulipa! Sijawahi kulipwa zaidi ya mil 3.5 na msanii yoyote Tanzania kama yupo aje nitampa video 10 buree. @rehemavisuallab @nisherbybee @jerrymushalastudios @hefemi @meckykaloka # niggarstalkingshit#mnanitibuasasa#noneducatedniggasoncrack#.”

Director Jerry Mushalla na yeye alicomment kwenye post ya Adam:
“Most Musicians like to blog and talk too much... But when it comes to actual payments they don’t pay… @adamjumanxl I wish directors woote mngekuwa na msimamo wa pamoja @hefemi @nisherbybee @abas_adam @travellah”.

Na hiki ndicho Nisher alichokisema wiki hii kuhusu swala hilo:
“Mi sipati logic wasanii wanavyosema wanaweza kulipa sijui milioni za hela wapi… mimi napigiwa simu na wasanii wakubwa lakini kila anayekupigia anasema mimi sina hela lakini, naweza kukugharamia chochote unachotaka tushoot video.

Unaanzaje na kauli halafu na wakati mimi nasoma kwenye internet kwamba umelipa sijui kiasi gani gani gani kwenye video fulani fulani, nafikiri video ya Ben Pol juzi tu ambayo tuliifanya ‘Unanichora’ labda ndiyo video niliyopata hela nyingi kwa kiasi fulani kwa sababu video iligharimu karibu milioni 10 hivi. Mimi nadhani tunachukuliana poa.

Kwa Mfano ukinilipa milioni 5 au 10, una uhakika kwamba hela hiyo hiyo itatumika kusambaza kazi yako […] kufanya kila kitu. Vyombo vipo cranes nini, cranes zenyewe za kukodi kwa siku laki 5, camera zipo za kukodi Red Camera unaambiwa labda dola 800 kwa siku, nani atakupa hiyo hela? Hivi vitu vinakatisha tamaa wasanii hawatukubali wanatuona kama hatujui.”

Hiki ndicho alichokisema Ommy Dimpoz wiki hii na kuwafanya madirector nao kuamua kufunguka:


“Biashara ya video ishaingia ushindani, kwahiyo kuna haja ya kuwekeza kwenye vifaa, mimi na uhakika hapa mtu ana mavifaa kibao unaenda kushoot Lushoto huko noma, wazungu wenyewe watauliza umeshoot wapi. Tuna maeneo kibao Zanzibar wapi wapi wapi ya kufanyia video, sio kwamba hatuna maeneo, maeneo tunayo lakini hatujawa na vile vitu. Kwahiyo ndiyo maana hata mtu pia unafikiria aha! sijui nishoot Zanzibar, lakini unawaza kumchukua labda GodFather au nani kumleta huku Tanzania ndiyo mziki.


Halafu mtu utakapoleta vifaa hivyo na uhakika hautaishia kwenye video tu, kuna matangazo, utakodi utafanyaje… Watu lazima waelewe kitu kimoja kwamba hakuna mtu anayependa kujitia gharama kama kuna uwezo wa kuepuka gharama, sio ufahari mimi nina vitu vingi vya kufanya sio kwamba nataka tu nikalipe dola elfu 30 kushoot video wakati nina uwezo wa kuokoa hiyo hela labda kulipa dola elfu 15 au elfu 10.

Wadau wanatusikia sie ndio wasanii wenyewe tunasema kwamba muziki unalipa mnaona sasa hivi vijana wenu wanapata shilingi mbili tatu, hizo shilingi mbili tatu mtagawana nao vipi kuliko kwenda kuwapa watu wengine huko nje ya nchi.
Jaji Vyonne Cherry au Monalisa akitoa maoni kwa washiriki waliokuwa wameshiriki kwenye filamu fupi iliyochezwa na washiriki wa TMT.
 Majaji wa Shindano la Tanzania Movie Talents (TMT) katikati wakiwasikiliza washiriki wa kundi la kwanza wanavyojielezea kabla ya filamu fupi waliyochezwa kuonyeshwa katika ukumbi wa Makumbusho ya Taifa wiki iliyopita
  Kundi la Kwanza la Washiriki wa TMT waliocheza filamu fupi iitwayo LUGHA GONGANA wakiwa mbele ya meza ya Pilato katika ukumbi wa makumbusho ya Taifa mwanzoni mwa wiki.
 Mshiriki wa TMT, Mwanaafa Mwinzago akifunika uso wake kwa kutoamini kuwa ameponea kwenye tundu la sindano kutokana na kuondolewa katika maumivu ya Jua la Utosi na kuendelea na mashindano hayo
 Mshiriki Wa TMT, Moses Obunde (Mwenye Suti) akimpongeza Mshiriki Mwenzie Mzee Kapalata Mtawa kwa kuweza kuondolewa Kwenye Jua la Utosi na Kupelekwa Kivulini katika Shindano la TMT linaloendelea.
 Washiriki walioingia kwenye Jua la Utosi wakiwa mbele ya Meza ya Pilato huku mshiriki mmoja kutoka kwa washiriki hao aliyaaga mashindano ya TMT.
 Simanzi Zikianzia hapo sasa mara baada ya Washiriki kupunguzwa ili apatikane mmoja wa kuondoka
 Wakabaki wawili na hatimaye mmoja kati ya hao aliweza kuondolewa katika mashindano hayo
 Hatimaye Mshiriki Isalito Isaya Akaweza kurudi ndani ya Mjengo wa TMT kutokana na Kura zake kumzidi Mshiriki mwenzie Pendo ambaye aliweza kuaga mashindano hayo kutokana na kura kuwa chache
Baadhi ya Washiriki wa TMT wakimuaga Mshiriki mwenzao Pendo Edward (Katikati) ambaye aliweza kutolewa kwenye mashindano kutokana na kura kuwa chache.Picha Zote na Josephat Lukaza

Na Josephat Lukaza - Proin Promotions Limited - Dar Es Salaam.

Hatua ya mchujo katika Shindano la Tanzania Movie Talents (TMT) limeingia wiki ya tatu ya mchujo sasa mara baada ya mshiriki mmoja kuaga shindano hilo wiki hii. Shindano la Tanzania Movie Talents (TMT) limekuwa shindano bora ambalo kadri siku zinavyozidi kwenda linazidi kuteka nyoyo za watanzania wengi waliopo ndani na nje ya Nchi kutokana na utofauti wake na uzuri wake pia.

Mshiriki mmoja ambaye ni Pendo Edward aliweza  kuchomwa na jua la utosi lililompelekea kutoka kwenye shindano hilo kubwa la Tanzania Movie Talents (TMT) ambapo mpaka sasa washiriki kumi na tano (15) ndio wamebaki katika nyumba ya TMT na hali ya simanzi bado inaendelea katika nyumba ya TMT kwa wiki hii ambapo mshiriki mwingine atatakiwa kutoka.

Shindao la TMT limekuwa likivuta hisia za watanzania wengi waliopo ndani na Nje ya Tanzania kutokana na Utofauti wake na ubora wake na kupelekea watanzania wengi sana kufuatilia shindano hilo kwa ukaribu na umakini zaidi.

Hatimaye wiki hii Tanzania Movie Talents iliamua kuzindua Zoezi la kuwapigia kura washiriki wake kupitia ukurasa wetu wa facebook ambapo sasa watanzania na wapenzi wa TMT ambao wanauwezo wa kupata na kutumia internet sasa wanaweza kuwapigia kura washiriki waliowavutia kupitia ukurasa wetu wa facebook na vilevile kuendelea kuwapigia kura washiriki kwa kutumia simu zao za mkononi.

Jinsi ya Kumpigia kura Mshiriki umpendae kwa Kutumia Simu ya Mkononi Andika Neno "TMT" ikifuatiwa na namba ya ushiriki halafu tuma kwenda 15678. Mfano TMT 00 tuma kwenda 15678

DSC_0741
Mgeni rasmi Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Iringa Dkt. Leticia Warioba ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Iringa akizindua rasmi kampeni ya SHUGA Redio ambapo amewaasa Vijana kuzingatia matumizi sahihi ya Kondomu na upimaji wa VVU ili kuzitambua afya zao mapema na kuepukana na maambukizi mapya ya VVU.
DSC_0757
Mkuu wa kitengo cha watoto na Ukimwi kutoka UNICEF, Alison Jenkins akizungumza kwenye uzinduzi huo ambapo amesema Lengo kuu la kampeni ni kusaidia juhudi za serikali katika kupunguza maambukizi mapya ya VVU miongoni mwa vijana wa umri wa kubalehe kupitia vyombo vya habari na kuwafikia kwa ujumbe mahususi kuhusu upimaji wa hiari na ushauri nasaha na ngono salama. Kampeni inakusudiwa kuchochea vijana walioko kwenye hatari kubwa ya kupata maambukizi waweze kutafuta na kuziendea huduma zilizopo.

Bi. Jenkins aliongeza kuwa kutakuwa na mfululizo wa vipindi 12 vya kuigiza wenye muda wa dakika nane umeelezea maisha ya vijana wanne (Sofia, Fally, Amina na Kavis) kuwakilisha vijana wa umri wa miaka 15 – 24. Simulizi iliyopo inahusu ndoto, chaguzi, marafiki, mapambano ya changamoto za kimaisha katika Dunia, ambayo UKIMWI ni tishio kubwa.Simulizi hizi kwa ujumla wake zinajikita kwenye somo la mbinu za upimaji wa VVU na ushauri nasaha, matumizi ya kondomu katika mahusiano ya muda mrefu , Kinga, unyanyasaji wa kijinsia na kingono, unywaji pombe na athari za kuwa na wapenzi wengi zinazopelekea kupata maambukizi ya UKIMWI.
DSC_0765
Mgeni rasmi Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Iringa Dkt. Leticia Warioba ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Iringa akimpongeza Mkuu wa kitengo cha watoto na Ukimwi kutoka UNICEF, Alison Jenkins (kulia) kwa risala nzuri wakati wa uzinduzi huo. Kushoto ni Kamishna wa TACAIDS na Balozi wa Vijana (UNICEF) na Kampeni ya SHUGA Redio, Faraja K. Nyalandu.
DSC_0694
Mratibu wa TACAIDS Mkoa wa Iringa, Bw. Owen Wimbo miongoni mwa wadhamini wa kampeni hiyo akizungumza machache na wakazi wa Iringa, Vijana na wageni waalikwa waliohudhuria sherehe ya uzinduzi wa kampeni ya SHUGA Redio iliyozinduliwa rasmi jana kwenye viwanja vya Samora mkoani Iringa.
DSC_0706
Kamishna wa TACAIDS na Balozi wa Vijana (UNICEF) na Kampeni ya SHUGA Redio, Faraja K. Nyalandu, akizungumza na vijana waliohudhuria uzinduzi huo ambapo aliwaasa kutouza mechi kusubiri muda muafaka na kuzingatia zaidi masomo sanjari na kuepuka kufanya ngono zembe.
DSC_0770
Mgeni rasmi akiwa ameungana na wasanii wa Bongo Flava pamoja na meza kuu kwa ajili ya kuzindua rasmi kampeni ya SHUGA Redio.
DSC_0774
Sasa imezinduliwa rasmi.....!
DSC_0653
Msanii wa muziki wa Bongo Fleva nchini Ben Paul akitoa burudani ya aina yake iliyoambatana na ujumbe mahususi wa kuhamasisha vijana kupima afya zao wakati wa uzinduzi wa kampeni ya SHUGA Redio ulioanyika jana mkoani Iringa kwenye viwanja vya Samora.
DSC_0931
DSC_0679
Umati wa vijana na wanafunzi wa shule mbalimbali za sekondari Iringa wakishuhudia burudani za wasanii maarufu wa Bongo Flava waliosinfdikiza uzinduzi huo.
DSC_0685
DSC_0793
Pichani juu na chini ni msanii wa muziki wa Hip Hop nchini anayejulikana kama Izo Business akitoa burudani kwa Vijana na wageni mbalimbali waliohudhuria uzinduzi wa Kampeni ya SHUGA Redio iliyozinduliwa rasmi jana mkoani Iringa kwenye viwanja vya Samora.
DSC_0815
DSC_0268
Baadhi ya wanafunzi wa Kituo cha Upendo mjini Iringa wakiwa kwenye foleni ya kuingia kwenye chumba maalum kwa ajili kupima Virusi vya Ukimwi bure wakati wa sherehe za uzinduzi wa Mradi wa SHUGA Radio uliofanyika kwenye viwanja vya Samora mjini Iringa.
DSC_0274
Mtaalamu kutoka AMREF akichukua vipimo vya damu kutoka kwa mmoja wa wanafunzi wa kituo cha Upendo mjini Iringa aliyejitolea kupima kwa hiari Virusi vya Ukimwi wakati wa uzinduzi wa Mradi wa SHUGA Redio unaotekelezwa kwa ushirikiano wa Mashirika ya Kimataifa moja linaloshughulikia Huduma za Watoto (UNICEF), Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) sambamba na Redio Jamii 10 nchini Tanzania wenye lengo la kuendeleza kampeni za hamasa kwa vijana kupunguza maambukizi mapya ya VVU.
DSC_0175
Vijana wa kiume nao walihamasika kupima afya zao bure bila malipo.
Pichani ni gari lillilopatwa na mkasa wa ajali nzito na habari yake inaanza kama ifuatavyo.

Kijana Joseph ambaye sasa ni marehemu enzi za uhai wake alibahatika kuwa na kazi nzuri kabla ya kuoa. Baada ya kuoa miaka mitano ya kwanza akabahatika kuwa na watoto mapacha wa kike na wa kiume na mke wake aliishi kwa furaha akifurahia baraka ambazo Mungu aliwapa familia ile.

Mke hakuwa na kazi na mme akaona ni vyema amsaidie kwa kumsajilia kampuni na mama yule akawa na kampuni ya mitindo na ikafana sana na kupata umaarufu katika eneo lile.

Miaka michache baadae baadae mme akapatwa na matatizo kazini na kusimamiswa kazi na kwa kuwa alikuwa daktari basi na leseni yake ya udaktari ikafungiwa na hakutakiwa kufanya kazi yoyote.

Mpango huo ulisukwa na wenzake pale kazini kwa kuwa alisifiwa sana kwa utendaji wa kazi zake na kupinga vitendo vya rushwa.

Maisha yakazidi kuwa mabaya pale nyumbani kwani miaka ilivyosogea hakupata tena wala kuliona lile penzi la mkewe, kwani mke akawa ni mtu wa kumchukia mmewe mara mme akihitaji fedha apewe kwa masimango na mbaya zaidi hata watoto wakaanza kufundishwa na mama yao kumchukia baba yao.

Hali ile ilimpa mzee yule wakati mgumu na ikafikia kipindi akaanza kudhohofika mwili kwa mawazo ingawa akajitahidi sana kutoyaonhesha hayo machoni pa matu na majirani.

Baada ya muda akapatwa na homa na akawa akijiuguza lakini baada ya muda akashauriwa aende akapimwe na kugundulika kuwa alikuwa na tatizo katika moyo wake lililosababishwa na msongamano wa mawazo.

Akamfuata mkeweofisini kwake na kumwambia anatyatizo la moyo na ilihitajika apate msaada wa fedha kiasi cha laki tano (500,000) kwa thamani ya fedha za kitanzania ili afanyiwe upasuaji wa haraka na kujiokoa katika hali hiyo hatarishi kwa maisha yake.

Mke alimjibu, " Sidhani kama nina hela ya kuchezea kwa kukupa mwanaume usiye na faida kwa familia yako... yaani mpaka chuni nikununulie mimi? Wanaume wenzako wanfanya kazi na sio kama wewe ulivyo sasa"

Baba alinyanyuka na kuufuata mlango bila ya kusema nen machozi yakimtoka na akikumbuka jinsi alivyoijenga familia yake kwa upendo na amani akiwapa mahitaji yote na jinsi alivyotumia mpaka tone lake la mwisho la fedha, muda na hata jasho kuinyanyua biashara ya mkewe ambayo ni kwa ajili ya familia.

Akawasha gari na kuondoka kuelekea nyumbani akiwa na mawazo huku akiona jinsi mtu umpendaye anayoweza kubadilika kiasi cha kukuombea ufe kwa kuwa ni kero kisa huna kazi na kumfananisha na wale wote.

Huku nyuma mke akaingiwa na roho ya ubinadamu na na kujilaumu kwa kauli ile na kuanza kuumia kisha akajaribu kumpigia simu mzee ikawa haipokelewi na kumka kuliwasha gari na kuanza kumfuata mzee
Kilomita chache mbele akaona kuna mkusanyiko mkubwa wa watu akapaki gari na kuuliza kuna nini? wakamwambia kuna ajali ya gari kuna mzee alikuwa anataka kuingia upande wa kushoto bila kuona kama kuna gari.

Kusogea pale hakuamini kuona mwili wa mme wake ukiwa umefunikwa alinianza kutokwa na machozi kabla ya kuingia kwenye gari na kuona kuna kadi nzuri ikiwa kwenye bahasha akaifungua na kuisoma.
Kilio kikubwa kilimtoka baada ya kugundua kuwa siku hiyo ilikuwa ni siku za kuzaliwa ya baba huyo na hakuna aliyekumbuka zaidi ya yeye mzee kununua kadi iliyoandkiwa " NAKUSHUKURU MUNGU KWA KUNIFIKISHA MWAKA HUU MPYA PAMOJA NA CHANGAMOTO NINAZOZIPITI NAAMINI KUNA SOMO WATAKA KUIPA JAMII KUPITIA MIMI. UHIMIDIWE BWANA... HAPPY BIRTH DAY TO ME"

Mama yule aliomboleza na mpaka sasa anazidi kuomboleza na hana amani tena hata faida ya ile biashara haioni tena na hajui nani atamsamehe.

1. Je unapitia mapito gani sasa katika mahusiano yako?
2. Je unayamudu vipi matatizo ya mahusiano yako?
3. Je unafikiria nini kama siku ukiamka na kuona wewe ndio chanzo cha kifo, kilema au chanzo msongamano wa mawazo kwa mwenza wako kutokana na tabia zako za ubinafsi?

Ndugu una kila sababu ya kumshukuru Mungu kwa kukupa mwenza huyo na kuamini kuwa katika kila mnalolipitia ni jaribu la kuwafanya muwe na sababu ya kuonyeshana upendo vyema zaidi ya ule wa mwanzo; Nimeumia sana mpaka nimefikiria sana mahusiano yangu na watu wanaonizunguka nikajiona nina kila sababu ya kusema R.I.P Joseph ni kupitia wewe umenipa somo la upendo na uvumilivu na kuzishinda stress za dunia hii.

R.I.P Joseph na kisha mshirikishe ujumbe huu uwape matumani wote walio katika migogoro ya mapenzi na wapendane kwani hakuna hali mbaya inayodumu zaidi ya kuwa mapito tu.

Imeletwa na Tabasamu na Fuledi
1. Huwezi kuwapenda watu wa nje kama huna mapenzi ya dhati kwayule uliyenaye kwenye uhusiano sasa.

2. Kumsaliti mwezio kwa kisingizio cha kulipiza kisasi huwa njia rahisi ya kukuingiza katika mgogoro binafsi na mwishowe kukuharibia kila mipango yako.

3. Kamwe usijidanganye kuwa utaweza kumsaliti na kumdanganya mwenzio kwa muda mrefu bila kugundulika, kila usaliti ni sawa na mimba lazima kuna muda utafika kila mtu ataiona tu.

4. Mahusiano yoyote hujengwa na uaminifu na kuthaminiana huku neno samahani na nimekusamehe likiwa nguzo kwa utatuzi wa kila tatizo mbele yenu.

5. Kusema nisamehe sio kuonekana mjinga bali pia huweza kukupa heshima na kuongeza mapenzi ya dhati baina ya yenu.

6. Neno nitakuacha au tuachane isiwe silaha ya kumwonea mwenzio maana nalo likizoeleka huweza kumfanya mwenza wako kuchukua maamuzi magumu kwani huashiria wewe una watu huko nje wakupao kiburi.

7. Kamwe usiwe mwepesi wa kuamini nini watu wanasema ila mshirikishe mwenzio kila uvumi ukoonyesha kumwamini na kumpa nafasi ya kukupa ufafanuzi.

8. Kila mahusiano huja na Baraka zake na huondoka na Baraka zake, unaweza ona unapata mafanikio sasa kwa sababu ya kuwa na huyo uliyenaye. Hivyo jitahidi kuzitazama kwa makini kila fursa njema upatazo na ona je zikiondoka utakuaje.

9. Fedha huleta ufahari lakini kamwe haina mchango katika kuleta furaha kwenye mahusiano yenu, hivyo pendaneni kama vile ni matajiri na maskini, kwani fedha yaweza kupotea muda wowote na kama mnapendana itarudi pia kwa kushirikishana jinsi ya kuirudisha lakini mapenzi yakiisha hata uwe na gunia la pesa ni kazi bure sawa na kuirudisha ladha ya chumvi siku ikiisha.

10. Mahusiano ya wawili hupendeza kama hayataingiliwa na watu wengine nanyi mkishirikishana katika kutatua matatizo na kuwa na maamuzi ya pamoja kwa kila jambo.

11. Ni vyema kutengeneza mazoea ya kujivunia na kuona ufahari kwa huyo uliyenaye na kama ukishindwa kuyafanya hayo kwa huyu hata ukimpata mpya mchezo utakuwa huo huo kwani bado huna ujuzi wa kuishi na mwenzako.

12. Huitaji kuwa dikteta kwa kuwa na misimamo ya kikoloni bila ya kuwa na utambuzi wa kuwa mko watu wa wili hivyo acha tabia za ubinafsi.

13. Wanawake wazuri na wanaume wenye mvuto hawawezi kwisha amini uliyenaye hukumpata kwa bahati mbaya, mpende kwa dhati.

14. Kila maamuzi ufanyayo sasa ukiwa na stress au huna sress huwa na tabia ya kuihaibu kesho yako, hivyo jitahidi kuwa na subira katika kila jambo.

15. Mapenzi hayaonyeshwi kwa kufungua zipu au kwa binti kupanua miguu tuu, mapenzi ni hisia, jinsi mnavyoishi, maelewano, ushirikiano na mambo mengine mengi.

16. Upendo hausubiri siku ya Valentine, kila siku ifanye kuwa siku ya valentine kwa mpenzi wako.

Imelewa kwenu na Tabasamu na Fuledi.
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Shehe Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Alhad Mussa Salum alipowasili kwenye makaazi ya Waziri Mkuu Mhe Mizengo Pinda (nyuma yao) Oysterbay jijini Dar es salaam kwa ajili ya Futari leo Jumamosi Julai 26, 2013. Kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam na wa pili kulia ni Kamanda wa Kanda Maalumu ya Polisi ya Dar es salaam Kamishna Suleiman Kova
 Rais Kikwete na Makamu wa Rais Dkt Mohamed Gharib Bilali wakijumuika na waumini wengine katika Swala ya Magharibi katika  makaazi ya Waziri Mkuu Mhe Mizengo Pinda Oysterbay jijini Dar es salaam alikoandaa Futari leo Jumamosi Julai 26, 2013
 Waziri Mkuu Mizengo Pinda akiongea na baadhi ya waalikwa kwenye futari aliyoandaa, wakiwemo waigizaji Mpoki wa Ze Komedy, Stephen JB, na watangazaji wa redio

 Makamu wa Rais Dkt Mohamed Gharib Bilali, Waziri Mkuu Mhe Mizengo Pinda, Jaji Mkuu Mhe Mohamed Chande Othman na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Dar es salaam Ndg Ramadhani Madabida wakipakua futari
 Waziri Mkuu Mstaafu Jaji Joseph Sinde Warioba akijumuika na waalikwa wengine kupakua futari
 Mawaziri wakuu Wastaafu Mzee Cleopa Msuya na Jaji Joseph Sinde Warioba wakiwa wameketi pamoja na Gavana wa Benki Kuu Profesa Benno Ndulu (kulia, mwenye baraghashia) na Mkurugenzi Mkuu wa PPF Bw. William Erio
  Kamanda wa Kanda Maalumu ya Polisi ya Dar es salaam Kamishna Suleiman Kova (kushoto) akiwa na viongozi wa dini Mchungaji wa Kanisa la Maombezi (GRC) la Ubungo jijini Dar, Lusekelo Antony 'Mzee wa Upako' (wa pili kushoto),  Rais wa shirika la kidini la Wapo Mission International Bishop Sylvester Gamanywa (kulia) na mashehe 
 Meza kuu ikifurahia jambo baada ya futari
 Meya wa jiji la Dar es salaam Dkt Didas Masaburi na Mwenyekiti wa Jumuiya ya wazazi ya Chama Cha mapinduzi CCM (Taifa) Bw. Abdallah Bulembo wakiwa na waalikwa wenzao kwenye futari hiyo
 Sehemu ya waalikwa
 Wazee Mashuhuri wa mkoa wa Dar es salaam mezani pao
 Mufti wa Tanzania Sheikh Shaaban Issa Simba akiongoza dua baada ya futari
 Sehemu  ya waalikwa kwenye futari hiyo
 Rais Kikwete akiagana na mmoja wa wazee mashuhuri wa Mkowa wa Dar es salaam
 Rais Kikwete, Makamu wa Rais Dkt Mohamed Gharib Bilal na Waziri Mkuu Mizengo Pinda wakisalimiana na waalikwa baada ya kufuturu pamoja
 Rais Kikwetena  Makamu wa Rais Dkt Mohamed Gharib Bilal wakisalimiana na waalikwa 
 Rais Kikwetena Waziri Mkuu Mizengo Pinda wakisalimiana na waalikwa baada ya futari
 Rais Kikwete akisalimiana na mchora katuni maarufu Ali Masoud 'Kipanya' huku Mrisho Mpoto akisubiri zamu yale
 Rais Kikwete akifurahi pamoja na waalikwa wenzie
 Rais Kikwete akisalimiana na mmoja wa wazee mashuhuri wa Dar es salaam
 Rais Kikwete akisalimiana na mwanamuziki Christian Bella
 Rais Kikwete akisalimiana na mwanahabari mkongwe Bw. Mwondosha Mfanga
 Rais Kikwete akisalimiana na mwanamuziki nyota wa kizazi kipya, Ommy Dimpoz
 Rais Kikwete akiongea na Mwana FA.
 Rais Kikwete akisalimiana na mtayarishaji, Muongozaji na mwigizaji nyota wa filamu Kulwa Kikumba 'Dude
Rais Kikwete akiendelea kusalimiana na waalikwa wenzie
Mkono wa mwisho ni wa mtoto huyu aliyepata bahati ya kuagana na Rais Kikwete na Makamu wa Rais Dkt Mohamed Gharib Bilali baada ya futari