Na Mwandishi Wetu.

Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe amesema wajumbe wa Bunge la Katiba kutoka katika chama chake hawatashiriki katika Bunge hilo linalotarajiwa kuendelea mwezi ujao.

Aidha, amesema Chadema haitashiriki katika kikao cha Julai 24 kilichoitishwa na Mwenyekiti wa Bunge Maalumu la Katiba, Samwel Sitta akisema hicho ni sehemu ya Bunge hilo ambalo wajumbe wake na wenzao wanaounda Umoja wa Katiba ya Watanzania (Ukawa) walilisusia.

Akisoma tamko la Kikao cha Kamati Kuu ya Chadema kwa waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Mbowe alisema iwapo Bunge hilo litapitisha Rasimu ya Katiba Mpya isiyotokana na maoni ya wananchi, chama hicho kikiwa sehemu ya Ukawa, kitafanya kampeni nchi nzima kuwashawishi wananchi kuikataa wakati wa upigaji wa kura ya maoni.

Alisema kuliko kupata Katiba Mpya ambayo ni mbovu ni bora mchakato wa kuipata uchelewe ili Ukawa waendelee kupigania Katiba bora itakayopatikana kutokana na maoni ya wananchi na siyo maoni ya CCM.
Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: